Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini

Hon. Nuru Awadh Bafadhili

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini

MHE. NURU A. BAFADHILI: Mheshimiwa Spika, awali ya yote nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa uhai na afya aliyonipa. Napenda kuipongeza Wizara kwa kufungua maduka mbalimbali ya kuuza madini.

Mheshimiwa Spika, kitendo cha ufunguzi wa maduka haya kitasaidia kupatikana madini yetu kwa wingi badala ya madini yetu kusafirishwa kwa njia za panya kwenda nje. Vilevile ufunguzi wa maduka haya utawasaidia wachimbaji wadogo kuweza kuuza madini yao na kupata fedha katika njia za usalama badala ya hapo awali baadhi walikuwa wanadhulumiwa haki zao.

Mheshimiwa Spika, kuhusu wachimbaji wadogo wadogo, wahamasishwe kuwa na vifaa vya uchimbaji siyo wachimbe kiholela. Wachimbaji hawa wadogo wahamasishwe kuuza madini yao katika masoko yaliyoanzishwa ili kuepuka kudhulumiwa haki zao. Serikali ihakikishe wenye maduka ya kuuza vitu vya dhahabu (sonara) wasichanganye madini wakati wanapotengeneza vitu hivyo mfano pete, vipuli (hereni), mikufu, vikuku na kadhalika.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.