Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini

Hon. Hasna Sudi Katunda Mwilima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini

MHE. HASNA S. K. MWILIMA: Mheshimiwa Spika, na mimi nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri na Naibau Waziri, Katibu Mkuu pamoja na watendaji wote wa Wizara. Leo mimi nitajikita kuzungumzia minerals (industries). Madini ya viwandani kama gypsum, lime stone, coltan nakadhalika. Madini ya viwandani yana soko zuri nje ya nchi hasa Afrika Mashariki. Kwa mfano limestone unaweza kusafirisha kwa kuiponda kuwa kokoto au ambayo imekuwa processes au wengine wanachoma zile kokoto na kusafirisha kwenye viloba.

Mheshimiwa Spika, tatizo ambalo wachimbaji wangine wanapata hasa wachimbaji wadogo ni pale wanapohitaji vibali vya kusafirisha madini ya viwandani inawawia vigumu. Kwa mfano wachimbaji wa Kigoma, Katavi na Rukwa, ili wapate vibali lazima wasafiri kuja Dodoma na inaweza kuchukua hata miezi 6 hadi mwaka bila kupata kibali.

Mheshimiwa Spika, natambua Serikali inapenda madini haya ya viwandani yauzwe hapa hapa nchini, lakini tatizo ni bei. Kwa mfano kokoto za limestone zinanunuliwa na wenye viwanda vya saruji na wanalipa 25,000 hadi 35,000 kwa tani ilhali ukipeleka nje ya nchi, kwa mfano Burundi na Rwanda unalipwa USD 150 per tone. Sasa unaweza kuona ni jinsi gani wafanyabiashara wakubwa wa viwanda wanavyowalilia wafanyabiashara wadogo. Tunaomba Wizara iweke kanda za kutoa vibali vya kusafirisha madini ili kurahisisha wafanyabiashara wa madini ya viwandani wasafirishe kwa wakati

Mheshimiwa Spika, la pili ni kuhusu uingizaji wa vifaa vya viwandani kama crusher machines, Grinding machines, processing machines etc. Tunaomba Serikali itoe exemption ili wachimbaji wadogo waweze kuingiza mashine hizi na kuchimba kwa kisasa zaidi kuliko ilivyo sasa, ambapo wanagonga mawe ili yawe kokoto ndipo wapange kumi kwa ajili ya kuchoma. Mkitoa vibali vya kuingiza hizi mashine utapunguza wachimbaji wadogo kuharibu mazingira kwa kukata miti.

Mheshimiwa Spika, mwisho ni kuhusu suala la grants najua kuna mikopo ya wachimbaji wadogo niombe Wizara iangalie na wachimbaji wa Kigoma kwani Jimbo langu lina wachimbaji wengi wa chokaa. Kwa leo mchango wangu ni huo.

Mheshimiwa Spika, mwisho niendelee kumpongeza Mheshimiwa Waziri Doto Biteko na Naibu wake Mheshimiwa Nyongo kwa kazi kubwa wanayoifanya kwenye Wizara hii naunga mkono hoja.