Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini

MHE. LUCIA U. M. MLOWE: Mheshimiwa Spika, naomba kuchangia hoja hii kama ifuatavyo; Mradi wa chuma wa Mchuchuma na Liganga. Nasikitika kwamba mradi wa Mchuchuma na Liganga uko kimia. Hata katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri haujatajwa. Mradi wa Mchuchuma na Liganga ungefanikiwa ungekuwa na manufaa makubwa sana. Kwanza ungewasaidia wananchi wa Mkoa wa Njombe kupata ajira pia pamoja na kuuza mazao yao. pia ingesaidia Serikali kujiingizia kipato chake. Lakini pia ingepnguza gharama kwa Serikali kununua chuma nje na badala yake chuma hicho kingesaidia hata ujenzi wa reli inayojengwa (Standard Gorge Railway). Naomba Mheshimiwa Waziri atakapohitimisha hoja yake alieleze Bunge ni kwa nini Mradi huo unasuasua?

Mheshimiwa Spika, wachimbaji wadogo wana changangamoto nyingi. Moja ya changamoto hizo ni kutokuwa na elimu ya kutosha juu ya namna ya kuwa na bima ambayo angewasaidia wanapopata majanga kama vile kufukiwa na kifusi; hivyo kwa kuwa hawana bima wakipata majanga familia zao zinabaki katika hali ya umasikini. Naiomba Serikali itoe elimu kwa wachimbaji hao ili kila mchimbaji awe na bima.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.