Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, napenda kuchangia Wizara hii ya Madini kulingana na umuhimu wake kwa vizazi vilivyopo na vijavyo katika kulinda rasilimali zetu za nchi yetu kwa kuzingatia mambo muhimu katika kuhifadhi rasilimali zetu.

Mheshimiwa Spika, Wachimbaji Wadogo. Kumekuwa na malalamiko makubwa kwa wachimbaji wadogo nchini. Nashauri Serikali kubadilisha utaratibu wa kuwatia moyo kwa kutatua changamoto zao kwa wakati kwani nao ni muhimu.

Mheshimiwa Spika, mikataba inayolalamikiwa ifanyiwe marekebisho. Kumekuwa na malalamiko kuwa kuna baadhi ya mikataba ambayo pia inafanya baadhi ya wawekezaji kuona kwao ni kikwazo kuja kuwekeza nchini. Ninashauri Serikali mikataba hiyo ipitiwe upya.

Mheshimiwa Spika, Tume ya Madini. Nashauri Serikali itimize wajibu wake kikamilifu kwani Tume hii ikitimiza wajibu wake kwa uhakika na kwa muda mwafaka kutaleta matokeo chanya kiutendaji na pia kulipatia taifa letu mapato kwani wataweza kutatua kero nyingi na baada ya kutatua tutaweka mazingira rafiki kwa wawekezaji wa ndani na nje.

Mheshimiwa Spika, Tume ya Utafiti ya Madini. Tume hizi ni vyema zikawa zinaleta matokeo yanayotokana na tafiti wanazozifanya kwenye maeneo mbalimbali nchini ili wananchi ambao si wataalam lakini wamekuwa wakigundua madini mbalimbali nchini. Ni vyema pia kuwatia moyo wananchi hawa kwenye maeneo mbalimbali hata kwa kuwapa maeneo ili kujua na kutambua michango yao.

Mheshimiwa Spika, kumekuwa na vifo mbalimbali kwenye maeneo ya uchimbaji kwenye maeneo au machimbo ambayo yamekuwa yakiathiri nguvu kazi ya Taifa. Nashauri Serikali kufuatilia kwa ukaribu mambo yanayopelekea vifo vya kila wakati kwa wachimbaji wadogo.

Mheshimiwa Spika, kutoa elimu maeneo yanayopatikana na uchimbaji wa madini. Kuna maeneo mengi ambayo wananchi wanaozunguka migodi. Serikali itoe elimu kwa wananchi juu ya athari ambazo wanaweza kupata kutokana na vifaa au sumu zinazoweza kutumika katika uchimbaji wa madini kwenye maeneo ambayo yanachimbwa popote nchini.

Mheshimiwa Spika, Soko la Madini. Nashauri Serikali itumie Umoja wetu wa Afrika Mashariki kama fursa kwa kufanya tafiti la soko kulingana na aina ya madini tuliyonayo nchini kwetu ili kuwasaidia wachimbaji wetu na kulisaidia taifa kwa ujumla. Hii itawanufaisha wananchi wanaozunguka maeneo yote ya uchimbaji madini nchini.