Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini

Hon. James Kinyasi Millya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Simanjiro

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini

MHE. JAMES K. MILLYA: Mheshimiwa Spika, naomba niwapongeze sana Wizara kwa ujumla wake kwa kazi kubwa wanayofanya.

Mimi ni Mjumbe wa Kamati hii najua kazi mnayofanya ni kubwa na kubwa na hongereni sana. Mheshimiwa Maftaha ameongelea wizi wa Mererani hapa ni kabla ya ukuta kujengwa. Mheshimiwa Rais baada ya kuona kwamba kuna wizi mkubwa ukuta ukajengwa kazi hii inafanyika vizuri ukuta umedhibiti uimarishaji wa kodi na ndiyo maana unaona kwenye takwimu ya Wizara baada ya ku-collect milioni 700 tu tuna-collect sasa almost two point three billion. Kwa hiyo hii ni kazi kubwa iliyofanywa na Serikali ya CCM, hilo ni moja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vilevile na mimi nishukuru kwa ajili ya ujenzi wa Mererani, ule ukuta umesaidia nchi sana watu wetu wamenufaika, utajili unaongezeka. Hapo awali tulikuwa tunabezwa Mheshimiwa Rais kafanya kitu gani bwana, CCM inafanya kazi gani; lakini niwaambieni kitu kimoja mimi kama Mbunge wa Jimbo linalotokana na Tanzanite utajiri wa watu wetu miongoni mwa watu wetu unaongezeka kwa kiasi kikubwa sana, Serikali imenufaika. Hata hivyo Mheshimiwa anajua changamoto mbili tatu ambazo nitazitaja, muda hautoshi.

Mheshimiwa Spika, pale kuna milolongo mikubwa sana, Mheshimiwa Waziri unakumbuka mwezi wa nne tulikuwa wote na Katibu Mkuu, naomba msaidie kuwepo na wafanyakazi wa kuongezeka pale ili ile milolongo ya watanzania waliokuwa tayari kulipa kodi basi ipungue. Ninaomba suala la maji, unakumbuka siku ile tuliongelea.

Mheshimiwa Spika, wenzetu wa Upinzani kidogo mimi nawashangaa. Ukurasa wa 14 wa hotuba yao ukiona, hawa watu wanasema nchi hii imekuwa shamba la bibi, ukurasa wa 14 ile aya ya kwanza. Lakini baada ya kurasa 13 baadae wanajisahau wanaanza kusema, ukurasa wa 27, Kampuni ya ACACIA iliyomiliki mgodi wa North Mara kunadhibitisha malalamiko ya muda mrefu ya wananchi na kwamba wamepigwa faini kubwa sana Mheshimiwa Waziri na Wizara ya Mazingira. Sasa watu hawa huku mnasema Serikali haya madini yameachwa kama shamba la bibi lakini huku mnaona Serikali inafanya kitu gani, ninyi tuwaamini kwa kitu gani? Niwaambie kwa awamu hii ya Tano, mara ya kwanza Mheshimiwa Rais; na wewe unajua mmesimamia haya madini umeunda Kamati mbili ya Tanzanite na Diamond unakumbuka umesimamia kwa hiyo awamu hii kipekee kwa kweli ni awamu ya kipekee mmeamua kulinda rasilimali za nchi yetu.(Makofi)

Mheshimiwa Spika, lingine, kuna Kamati iliyochunguza mambo ya Tanzanite, kuna madeni ya ajabu ambayo yamelimbikiziwa watu wangu ma-Broker halafu wachimbaji wakubwa na wale ambao wanafanya masuala ya Tanzanite. Kamati hii imeamua kuchukua almost miaka kumi iliyopita kuwalipisha watu wangu madeni ambayo hayapo kabisa. Watu hawa wamekuwa ni maskini wengine hawana hata chochote. Mbali na uchunguzi uliofanyika kwenye Gold, mbali na uchunguzi uliofanyika kwenye masuala ya Diamond wameshikwa watu wa Tanzanite peke yake nchi ndiyo wanaosumbuliwa na Kamati fulani ambayo naomba nisiitaje na Mheshimiwa Waziri unajua na malalamiko yangu kama Mbunge nimeshakuambia niombeni mshughulikie kwa sababu uonevu huu haukubaliki hata kidogo.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema haya naunga mkono hoja, ahsante sana.(Makofi)