Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini

Hon. Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Awali ya yote nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa kibali cha kuweza kusimama na kuweza kuchangia hotuba hii ya Wizara ya Madini.

Mheshimiwa Spika, nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais Dkt. John Joseph Pombe Magufuli kwa kazi nzuri ya kuamua kujenga ukuta Mererani. Nilipongeze Jeshi, nimpongeze Mkuu wa Majeshi, General Venance Mabeyo, kwa usimamizi mzuri wa ujenzi huu wa ukuta wa Mererani. Tumeona ndani ya miezi mitatu Jeshi limeweza kujenga kilometa 24.5 na kutumia gharama ndogo ya bilioni 5.2 ambazo kwa mkandarasi wa kawaida Serikali ingeweza kutumia zaidi ya bilioni nane na kutumia muda mrefu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pongezi hizi si bure tu, tumeweza kuona matunda ya ukuta huu wa Mererani na tumeona kwamba mapato ya Tanzanite yameongezeka kutoka milioni 700 kwa mwaka, na katika taarifa ya Mheshimiwa Waziri amesema mpaka kufika Machi, mapato ya Tanzanite yameongezeka mpaka bilioni 1.43 na hivi sasa ninavyozungumza mapato ya Tanzanite yameongezeka mpaka bilioni 2.3. Hongera sana Wizara ya Madini kwa kazi nzuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niendelee pia kumpongeza Mheshimiwa Waziri wa Madini kwa kazi nzuri anayoifanya ya kusimamia uanzishwaji wa masoko ya madini. Ndani ya muda mchache wa miezi miwili tumeona kwamba wameshaweza kufungua masoko 13 ndani ya nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, pamoja na kuanzishwa kwa masoko haya, nilikuwa na ushauri katika Wizara hii ya Madini.

Mheshimiwa Spika, kwanza; Mheshimiwa Waziri na timu yako mhakikishe kwamba mnasimamia vizuri masoko haya ya madini ya kuhakikisha kwamba yanatimiza lengo lililokusudiwa na yasiende kugeuka kuwa kichaka cha wafanyabiashara haramu wa madini. Vile vile niwashauri Wizara hii muendelee kuwafanyia utafiti wa madini wachimbaji wadogo ili kuweza kuwapunguzia gharama ya uchimbaji. Vilevile endeleeni kuwatengea maeneo mengi wachimbaji hawa wadogo wa madini na ambayo yameshafanyiwa utafiti ili kuweza pia kuwapunguzia gharama za utafiti wachimbajia hawa wadogo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia niiombe Serikali iwasaidie wachimbaji wadogo katika suala zima la environmental impact assessment kule kwenye maeneo yao ambayo wanachimba madini. Muhakikishe kwamba mnawaelekeza namna bora ya kuchimba madini lakini wakati huo huo wakiwa wanatunza mazingira.

Mheshimiwa Spika, nizungumzie suaa la mradi wa Liganga na Mchuchuma. Mimi na Watanzania wengine hususan wakazi wa Mkoa wa Njombe Wilaya ya Ludewa tungependa sana kujua hatma ya mradi huu wa Liganga na Mchuchuma, kwani tumeweza kusikia mambo mengi mazuri yanayotokana na mradi huu lakini vilevile mradi huu umekuwa ni kichocheo kikubwa katika uchumi. Kwa sababu mradi huu endapo kama utamalizika utatoa ajira za moja kwa moja kwa watu 5,000 lakini ajira ambazo indirect kwa maana ya kwamba ya wakandarasi na jamii ambayo inazunguka mradi ule watu 30,000.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vile vile mradi huu kama utakamilika utaenda kuchangia Pato la Taifa (GDP) asilimia tatu mpaka asilimia nne. Hivyo basi na sisi wananchi wa Mkoa wa Njombe tuna hamu ya kuyaona mafanikio hayo na hivyo tunaiomba Seri kali iweze kutuambia status ya mradi huu iko vipi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimalizie tu kwa kusema, huu ni mradi wa kielelezo wa mpango wa miaka mitano kuanzia mwaka 2015 mpaka 2016 na 2020 mpaka 2021; lakini mpaka sasa ninavyozungumza hapa takriban miaka minne imeshapita na umebaki m wak ammoja tu hivyo basi kilio chetu wananchi wa Mkoa wa Njombe hususana Wilaya ya Ludewa tunaomba kujua status ya mradi huu Mheshimiwa Waziri ukija kufanya wind up, na kinyume cha hapo kwakweli utanisamehe Mheshimiwa naweza nikaja kushika shilingi.

SPIKA: Ahsante sana kwa kutumia muda wako vizuri sana.

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.