Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa kuchangia katika Wizara hii ya Maliasili na Utalii. Nianze kwa kuunga mkono hoja hii na kuwapongeza sana Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii pamoja na Naibu wake na viongozi wote wa Wizara hii, kwa kazi nzuri wanayoifanya hususan katika ulinzi wa maliasili zetu na vyanzo mbalimbali vya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimesimama kuchangia hoja kwa dakika chache ambazo umenipa, lakini nikirejea hutuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani kuanzia ukurasa wa 18 ambayo imeelezea muktadha mzima wa Rufiji hydropower na nimshukuru Naibu Waziri wa Fedha amesema, sitarejea katika upande lakini nimpongeze sana wake.

Ninachotaka kuwaomba Watanzania na Waheshimiwa Wabunge, kwa kuwa mradi umeanza na tunatarajia mwezi wa Saba kuweka jiwe la msingi na kazi mbalimbli za mazingira wenzeshi, masuala ya mobilization tayari, nadhani itakuwa ni kupoteza muda kuanza kuujadili kwa misingi ya kwamba turudi nyuma, haturudi nyuma. Hilo nataka niliseme wazi kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nataka nirejee kulitaarifu Bunge lako na nilipata kusema, mradi huu mradi huu ulifanyiwa tafiti mbalimbali na kimsingi tafiti zote hakuna tafiti ambayo iliainisha kwamba mradi huu hauna faida yoyote. Kwa sasa tunapotekeleza mradi huu imeshafanyika environment social impact assessment imeshafanyika strategic environment assessment ambazo wenzetu wa Maliasili wanaweza kulisemea vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo ninachotaka kusema sisi tumeangalia faida na hasara zake na hususan kwenye kwenye kumpunguzia mtanzania gharama kubwa ya matumizi ya umeme. Tumetathmini vyanzo mbalimbali na kwa kuwa tunatekeleza mpango kabambe wa umeme ambao umeainisha kila chanzo kinatakiwa kizalishe megawatt ngapi ili kufanya ile energy mix ya nchi iwe stable.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo nataka nilitaalifu Bunge lako Tukufu kwa kweli kwa namna ambavyo chanzo hiki cha maji kinagharimu shilingi 36, umeme unazalishwa na gesi unagharimu shilingi 147 umeme unazilishwa na mafuta unazalisha Sh.526. Pia ukiangalia gharama za uwekezaji, unapowekeza kwa kutumia imetajwa joto ardhi unatumia Sh. 10,039 kwa megawatt moja tofauti na unapowekeza kwa kutumia maji watumia Sh.6,000 kwa megawatt moja, kwa hiyo utaona hata gharama za uwekezaji zina nafuu kwenye miradi ya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho, chanzo cha joto ardhi Serikali ya Awamu ya Tano imewekeza, Wizara ya Fedha imeleta bilioni 32 kununua mitambo ya uchongaji wa visima vya majaribio. Kwa hiyo nataka niseme kwa kweli kwa Serikali yetu kwa energy mix inayoendelea tuna imani kabisa mradi huu mkubwa wa Rufiji hydropower utakaozalisha megawatt 2115 ndiyo mkombozi kwenye uchumi wa viwanda, lakini lile lengo la Rais wetu, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli ya kupunguza gharama ya umeme kwa watumiaji wa kawaida na viwandani litatimia kwa kuwa itakuwa ndiyo mradi mkubwa wa kwanza.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivi nchi mbalimbali zilizoweza kujenga mabwabwa makubwa, ikiwemo Ethiopia ikiwemo Unganda, na nchi nyingine zimewezaje na sisi tushindwe kwa ajili tu ya masuala ya mazingira? Kwa hiyo, nikuthibitishie sisi watekelezaji Wizara ya Fedha imetuwezesha, tunaendelea kusimama mradi huu kwa maslahi ya nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)