Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nianze kwa kukushukuru kwa kunipa fursa hii ili nami nichangie hoja iliyowekwa mezani na Mhehimiwa Waziri Maliasili na Utalii. Nianze kwa kuunga mkono hoja hii, lakini pia kuwapongeza sana Waheshimiwa Waziri na Naibu Waziri wake kwa kazi nzuri wanayoendelea kuifanya.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa muda ni mchache naomba niseme hili suala kikodi na tozo kama ambavyo nimekuwa nikisisitiza siku zote nashukuru tumelipokea, tumelisikia wamesema, lakini niendelee kuomba tusiwahishe shughuli, tusubiri muda wa shughuli hii ukifika tutaongelea kuhusu tozo na kodi mbalimbali.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la pili ambalo ningependa kulitolea maelezo machache ni hili kwamba Serikali ilikataa ofa iliyotolewa na Serikali fulani kwa ajili ya utekelezaji wa mradi mbadala wa mradi wa kuzalisha umeme wa Mto rufiji. Naomba niseme yafuatayo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kulingana na Sheria ya Misaada, Mikopo na Dhamana, ni Wizara ya Fedha pekee inayoshughulikia mikopo, dhamana na msaada kutoka sehemu yoyote ndani ya dunia hii na wanaposimama Mheshimiwa Mbunge kusema kwamba Serikali ilipata offer na ikakataa tuwe tunajitathimini, kujitafakari nini tunakisema na lengo letu la kusema jambo hili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunapopata taarifa ya aina hiyo sisi kama Wizara rasmi huwa tunapeleka kwenye Kamati yetu ya Taifa ya Madeni kufanyia analysis ya huo unaoitwa msaada au offer. Tukishamaliza kwenye Kamati ya Madeni, wanamshauri Mheshimiwa wa Fedha. Sasa unapofika kwenye conclusion, unasimama kwenye Bunge Tukufu kuwadanganya Watanzania dhamira yako ni ipi? Hilo lazima tulielewe. Sisi kama wenye Wizara yenye mamlaka ya kushughulika na misaada, mikopo na dhamana hatujawahi kupata formal letter yoyote kutoka sehemu yoyote ndani ya dunia hii kwa ajili ya utekelezaji wa mradi mbadala.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, niwaambie Watanzania weendelee kumpuuza Mheshimiwa Mbunge huyu ambaye amesimama akiwa amepewa dhamana kuja kuwadanganya Watanzania. Dhamira ya Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli ni njema sana. Tunakwenda kwenye Tanzania ya viwanda, tunatekeleza Mpango wa Pili wa Maendeleo, Dira ya Taifa letu 2025, kujenga uchumi wa viwanda utakaoleta mabadiliko kwa wananchi wetu, lazima tuwe na umeme wa bei nafuu, lazima tutekeleze mradi huu na naomba niseme tuko tayari na tumeanza kutenda.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia amesema Mhehimiwa Mbunge huyu kwamba Serikali haina uwezo, naomba nimwambie tumejipanga, tumejiandaa na tupo tayari kutekeleza mradi huu na utakamilika kwa wakati na Watanzania waweze kufaidi matunda ya Taifa lao. Ni jambo dogo la kawaida la kujiuliza amesema vizuri Mheshimiwa Dkt. Mollel. Daktari Mollel alipoulizwa ni wao taifa hilo hilo ambalo walisema miaka hiyo kama ungetekelezwa mradi huo ungekuwa ni chanzo kikubwa cha maendeleo ya Taifa lao. Leo kuna nini Watanzania tunatekeleza wenyewe?

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tusikubali kutumika bila kuwa na sababu ya msingi, sisi ni Taifa huru, tumesimama na mradi huu tutautekeleza na naomba niliambie Bunge lako Tukufu tayari tumshapeleka Sh.688,650,898,267 kama fedha ya kuanza utekelezaji wa mradi huu na pesa yake ipo wala hatuhitaji kwenda kukopa au kuomba, ipo kwa ajili ya mradi wa umeme wa Mto Rufiji.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la mwisho…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana na narejea kusema naunga mkono hoja hii.