Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Dr. Haji Hussein Mponda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja ya Waziri na niwapongeze Mawaziri pamoja na timu yao yote ya Wizara katika kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naishauri Wizara katika kupanua wigo wa mazao ya utalii kwa kutumia Mto wa Kilombero kwa utalii wa kuvua samaki wakubwa aina ya Mjongwa n.k.; yaani king fish touring katika Mto Kilombero. Utalii huu ulikuwepo hapo mwanzo lakini hivi sasa umesimama kwa muda mrefu, inahitajika promotion kubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la utatuzi wa mgogoro wa matumizi ya ardhi kati ya hifadhi/vijiji. Napongeza Serikali katika jitihada zake kwa kukabiliana na migogoro hii; shukrani za pekee kwa Mheshimiwa Rais kwa hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na utoaji wa elimu ya uhifadhi, uhakiki wa mipaka katika Pori Tengefu la Kilombero, nashauri Serikali, katika vijiji 16 ndani ya Wilaya ya Malinyi zoezi hili la uwekaji alama za kudumu/uhakiki wa mipaka irudiwe tena kwa kuwa mashamba mengi ya wanachi wa Malinyi kwa sasa yapo katika ardhi ya Pori Tengefu la Kilombero. Hivyo, kusababisha uendelezaji wa mgogoro wa wananchi wa vijiji hivyo na pori tengefu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaishauri tena Serikali, kwamba ingerejea upya zoezi la utambuzi wa mipaka/ uwekaji wa alama za kudumu ili kuyanusuru mashamba ya wananchi kwa maendeleo na ustawi wa wananchi lakini pia uendelezaji wa uhifadhi. Ahsante.