Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichangie katika hoja hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, tozo nyingi; kwenye sekta hii ya utalii kuna tozo nyingi mno. Serikali ipunguze kodi hii ili iwe kama kivutio cha kupata watalii wengi ambao watatuingizia fedha za kigeni za kutosha.

Mheshimiwa Naibu Spika, Migogoro Baina ya Serikali na Wananchi. Kwa kuwa kuna migogoro kwa wananchi wanaoishi karibu na hifadhi za wanyama, Serikali ijitahidi kutatua migogoro hiyo hata kama Wizara imejitahidi kupunguza kwa kiasi kikubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Vivutio vya Utalii – Njombe. Ninaomba Serikali ivitambue vivutio vya kiutalii katika Mkoa wa Njombe ili kuliingizia kipato taifa letu. Vivutio hivyo ni Mapango ya asilia yaliyoko katika Halmashauri ya Njombe Mjini eneo la Nyumbanitu. Eneo hilo lina kuku wa ajabu na vivutio vya kale. vilevile Mbuga za Kitulo ambapo kuna maua ya kila aina, jiwe lenye ramani ya Afrika asilia, maporomoko ya Mto Mwihe na Lupali – Njombe. Naomba Serikali ifuatilie mambo hayo na kisha kupeleka watalii.

Mheshimiwa Sika, Bajeti. Kwa kuwa sekta hii ya utalii ni muhimu sana katika kukuza uchumi wa taifa letu basi Serikali ihakikishe fedha inayoidhinishwa na Bunge itolewe kwa wakati na itolewe yote.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.