Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Naibu Spika, matukio ya wanyama waharibifu hasa tembo na nyati waliharibu mazao ya wananchi katika Vijiji vya Rhotia, Kilimatembo, Ayalabe, Kitete, Kamba ya Nyoka na Oldeani Wilayani Karatu yamekuwa ya kujirudia rudia na mwaka huu yamekithiri.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivi sasa tembo wengi wanashinda mashambani na kula mahindi ambayo bahati mbaya mwaka huu yako kidogo sana; wanyama hao wanatoka Hifadhi ya Ngorongoro. Niishauri Serikali iwaelekeze mamlaka hiyo kuongeza doria ili kuwadhibiti wanyama hao.

Tembo hawasikii lolote, wananchi wanahangaika sana na mazao yao yanaharibiwa sana. Katika ukanda huo wa msitu kuna kambi tatu tu. Kambi hizo hazitoshi na pia askari wawe na mafuta na silaha zote.

Mheshimiwa Naibu Spika, wako baadhi ya askari wa wanyamapori ambao wanaendeleza uonevu na ukatili kwa mifugo inayoingia kwenye hifadhi kwa bahati mbaya. askari hao wamekuwa wakiua au kujeruhi ng’ombe. Hivi majuzi askari wa hifadhi ya Ziwa Manyara waliwaua ng’ombe watatu na kujeruhi wengine watano na pia kumvunja mguu mwananchi kwa kumpiga risasi mguuni.

Mheshimiwa Naibu Spika, ng’ombe hali wanyama wala hashambulii wala kudhuru miti kwanini wapigwe risasi? Askari hao si waadilifu kabisa na wamekuwa wanapokea rushwa ili mtu aingize mifugo. Huo ni unyama dhidi ya mifugo.

Mheshimiwa Naibu Spika, siku za nyuma NCAA na TANAPA walikuwa wanasaidia miradi mbalimbali ya maendeleo; tangu mwaka 2016 miradi hiyo imepungua sana. Ili waone kuwa na wao ni sehemu ya hifadhi hizo ni vyema miradi ya maendeleo ya wananchi iweze kutekelezeka, kama vile miradi ya shule, afya, maji na kadhalika.