Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, Kuhusu Misitu. Kwa dhati ya moyo wangu nawapongeza sana mmejitahidi sana kuiinua sekta na kuleta utulivu katika sekta na hasa suala zima la upatikanaji wa malighafi katika Shamba la Sao Hill. TFS na uongozi wa Shamba la Sao Hill wamekuwa na ushirikiano mzuri na Halmashauri ya Mji wa Mafinga hasa katika Corporate Social Responsibility na suala la ushirikishwaji wa wadau. Naomba suala hili la kushirikiana wadau na sisi viongozi wa kuchaguliwa liwe sustainable, na ni vizuri kila mara kabla ya mgao kuanza vikao viwepo ili wadau na sisi viongozi wao tuwe na uelewa mmoja.

Mheshimiwa Naibu Spika, Pamoja na hayo nina hoja kadhaa; Kuhusu Kuruhusu Mazao ya Misitu Kusafirishwa Masaa 24. Hili suala tumeshalileta na wakati wa kujibu swali langu la msingi na nyongeza tarehe 04 Aprili, 2019 Serikali Waziri na Naibu Waziri walilieleza Bunge kwamba jambo hilo liko katika hatua ya mwisho, nilitarajia suala hilo liwemo kwenye hotuba yako. Ombi langu ni kuwa tusikie kuhusu jambo hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kuhusu Mikataba kwa Wavunaji. Pamoja na mchango wangu wa maelezo ya mdomo bado ninawasilisha suala hili na pia natahadharisha badhi ya viongozi wa vyama vya wavunaji wanatumia fursa vibaya kwa kuendelea kujilimbikizia vibali. Yapo malalamiko mengi, ni muhimu kadiri tunavyoingia kwenye uwazi hali na ujanja ujanja huu umalizwe ili sekta iendelee kuwa na utulivu. Hata mtakapofikia hatua ya kuwapa wavunaji mikataba iwe ni wale ambao ni genuine na wavipate kwa uhakika na uwazi. Suala hili litafanikisha na kuongeza mapato kwa kuwa itawapa uhakika wa kukopa na kuajiri ipasavyo wafanyakazi ambao watachangia kupitia PAYE, SDL nakadhalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kuhusu Single Entry. Katika zama hizi za eGovernment – TEHAMA ni muhimu sasa kuliangaia suala hili kwa umakini ili kuziwezesha jamii zinazozunguka mbuga zetu kunufaika na utalii. Vilevile pia kuwapa uhakika wa kipato wananchi ambao ni sehemu ya ulinzi dhidi ya ujangiri. Mimi ni mdau wa utalii na familia inaendesha VAMOs Hotel Mikumi na Mafinga, pale Mikumi, Tungamalenga na maeneo ya aina hiyo uchumi umelala kwa sababu watalii wanapita juu kwa juu na hivyo kuondoa fursa ya kipato cha wananchi wa kawaida.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kuhusu Chuo cha Misitu – Olmotonyi Kuwa na Campus ndogo Mafinga. Naomba kuwasilisha tena ombi hili ambalo mkirejea michango yangu ya nyuma, nilishawasilisha; naomba mlitafakari.