Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

3

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Naibu Spika, hoteli zote zilizokuwa za Serikali zilizopewa, zilizokodishwa au zilizouzwa zifuatiliwe mikataba yake na utekelezaji wa mikataba kwa kuangalia hali za hoteli hizo na utendaji kazi wake kwani hoteli nyingi zinaonekana kuwa na hali mbaya na haziingizii faida Serikali na nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, TFS iendelee kuimarisha ushirikiano wake na jamii kwa kuondoa migogoro iliyopo kati yake ni vijiji kama kule Korogwe kwenye Hifadhi ya Nilo na Msitu wa Chang’andu, Kata ya Kwalukonge.

Mheshimiwa Naibu Spika, TFS na Wizara kuendelea kuacha kiwanda cha mazao ya misitu cha TAMISO CHIPBOARD ambacho bado kina mashine nzuri kimeendelea kuchezewa.

Mheshimiwa Naibu Spika, utetezi wa TFS na Wizara kuwa kiwanda hicho kinaangaliwa na Msajili wa Hazina sio sawasawa kwani hata uanzishwaji wa kiwanda hiki ulikuwa maalum kwa ajili ya mazao ya misitu ya shamba la miti la Shume na Gologolo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuendelea kukitelekeza kiwanda hiki ni matumizi mabaya ya fedha za nchi na kufifisha nia na dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na kazi nzuri ya kupambana na ujangili kumekuwa na ongezeko kubwa la tembo na wanyama wakali. Je, mamlaka zinazohusika zimejiandaaje kupambana na ongezeko hilo?