Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Suzana Chogisasi Mgonukulima

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. SUZANA C. MGONUKULIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2016 tembo walishambulia mashamba ya wananchi ya Mkoa wa Iringa, Wilaya ya Kilolo, Kijiji cha Mgowelo ambapo zoezi la kuhakiki lilifanyika lakini hadi leo hii hawajalipwa na uharibifu ulikuwa mkubwa, hakuna mwananchi aliyeambulia kitu chochote, wananchi hawa walipata shida kubwa sana ya chakula.

Mheshimiwa Naibu Spika, Sheria ipo wazi shida ya kutowalipa watu hawa ni nini? Kwa kuwa ni haki yao kulipwa, nimwombe Mheshimiwa Waziri wa mwenye dhamana wakati wa kuhitimisha hoja ya Wizara hii atoe majibu juu ya hatma ya wananchi hao.