Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, utalii na fursa ya watalii ambao ni askari wa UN wanaolinda amani kupitia UN – Mission; kuna kundi kubwa la askari ambao wako kwenye UN – Mission mbalimbali katika eneo la Maziwa Makuu na pia pembe ya Afrika. Nitafafanua kidogo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, DRC kuna Mission ya MONUSCO na Central Africa kuna MINUSCA. MONUSCO tu ina takribani watumishi 16,000, wengi wao askari kutoka Mataifa kama Pakstani, Bangladesh na Nepal. MINUSCA ina wafanyakazi zaidi ya 12,000, kutokana na mazingira ya kazi kila baada ya kipindi fulani hupewa likizo. Kwa sababu ya umbali wa kwenda makwao wengi hupendelea kwenda maeneo jirani kupumzika ikiwemo Zanzibar.

Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto; kwa sababu ya utaratibu wa Visa Rejea (Referred Visa) ambayo maombi yake huchukua muda mrefu na wakati mwingine hakuna majibu. Tunawapoteza watu hao ambao sasa wanakwenda Rwanda, Kenya na Uganda. Hili soko kubwa ikiwa mtu huyo ameshafanyiwa vetting katika level ya UN na ana passport ya UN, tunakosaje kuwa na utaratibu maalum. Tufikirie kwa mwaka tukiwapata japo 5,000 tu ni mapato kiasi gani. Ikizingatia kuwa hawa ni wale ambao High Value Tourism na ni long stay kwa sababu watakaa muda mrefu mpaka likizo yao itakapokwisha ambayo huwa ni wastani wa siku 14 mpaka 21.

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri; Serikali kupitia Wizara husika ya Mambo ya Ndani (Uhamiaji) na Mambo ya Nje na wao washirikiane kuona kuwa tunafaidi fursa hii.