Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchangia Wizara hii ya Maliasili na Utalii kwa kuwa ni Wizara ambayo ni muhimu sana kwa kuliletea Taifa letu fedha za kigeni.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la katazo la kutumia mkaa; bado kuna changamoto kubwa katika ukamataji, naomba Wizara hii ishirikiane na Wizara ya Muungano na Mazingira kwa Maafisa Mazingira pamoja na Maafisa Misitu.

Mheshimiwa Naibu Spika, migogoro kati ya wananchi na maeneo ya reserve; kumekuwa na malalamiko ya muda mrefu kwa wananchi wetu katika maeneo yao ambayo yanazunguka reserve. Ni vema Wizara hii ya Maliasili na Utalii kushirikiana na Wizara ya Ardhi ili kupima maeneo yao na kutatua migogoro hiyo ya muda mrefu.

Mheshimiwa Naibu Spika, sheria ya kifuta jasho imepitwa na wakati. Ni vyema Serikali ikaleta sheria hii Bungeni ili ifanyiwe marekebisho kwani imepitwa na wakati. Ni vema Wizara ikachukua hatua ya haraka kwani wananchi wana malalamiko ya muda mrefu kuhusu mazao yao yanayoliwa na wanyama, lakini kifuta jasho hakikidhi athari zinazowakabili baada ya mazao kuharibiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, maporomoko ya Kalambo; Wizara ichukue hatua kwa maporomoko haya kwani tunatumia nchi mbili lakini nchi ya Zambia inafaidika zaidi. Naomba kushauri Serikali kuwekeza fedha kwenye maporomoko haya ili na sisi tunufaike kama Taifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, tubadilishe aina ya matangazo yetu ya utalii.