Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. ENG. GERSON H. LWENGE: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote naunga mkono hoja hii na nampongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na viongozi wa Wizara hii kwa kazi nzuri ya kusimamia majukumu ya Wizara hii. Mwaka jana wakati wa kuwasilisha hoja ya bajeti kwa Wizara hii nilichangia kuhusiana na kuwepo kwa Pori la Akiba la Mpanga/Kipengele lilianzishwa mwaka 1995; wananchi wa vijiji 14 vya Wilaya ya Wanging’ombe walihamishwa kupisha uanzishaji wa pori hili la akiba, walilipwa fidia na mipaka iliwekwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi hao wamejenga nyumba za kudumu, shule, majengo ya ibada na kadhalika. Hivi karibuni Mamlaka ya TANAPA wamekuja kuweka vigingi tofauti na mipaka ya awali bila kuwahusisha wananchi au viongozi wa wilaya. Jambo hili limeleta taharuki na hivyo kuzusha mgogoro mkubwa. Jambo hili nilimfikishia Mheshimiwa Waziri ili achukue hatua ili wananchi hawa waishi kwa amani na vilevile azma ya kuwepo hifadhi ya pori la akiba iwe endelevu. Nilitarajia ningeona lolote ndani ya hotuba hii, lakini sijaona mpango wowote uliopo kwa ajili ya pori hili la Mpanga Kipengere, kwa hiyo, lipolipo tu. Basi kama ni hivyo naomba ramani ya awali iheshimiwe na vijiji hivi vilivyosajiliwa viachwe viendeleze maeneo yao. Vijiji hivyo ni Moronga, Kipengele, Imalilo, Ikanga, Wangama, Masage, Malangali, Wagamiko, Mpanga, Luduga, Hanjawanu, Igando, Iyayi na Mayale.

Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza sana Rais wetu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa tamko lake alilolitoa kwa vijiji vile vyenye migogoro na wananchi kwamba, Wizara iende kutatua migogoro ikihusisha wananchi, Serikali za Wilaya na ikikupendeza kumshirikisha Mbunge wa Jimbo. Nina imani agizo la Rais linahusisha pia mgogoro uliopo kati ya Hifadhi ya Pori la Akiba la Mpanga/ Kipengele na wananchi wa vijiji hivi 14 nilivyovitaja.