Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. RHODA S. KUNCHELA: Mheshimiwa Naibu Spika, uchambuzi na utekelezaji wa bajeti; makato ya mshahara zaidi ya shilingi bilioni 168 kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii ambayo hayakupelekwa katika taasisi husika (CAG Ripoti ya Ukaguzi wa Serikali Kuu 2017/2018 ukurasa 189).

Mheshimiwa Naibu Spika, Taasisi ambazo hazina mpango wa matengenzo na kumbukumbu za matengenezo ya mali za kudumu (Maliasili na Utalii) ukurasa wa 287. Kwa mujibu wa CAG mwaka wa fedha 2017/2018, Wizara ya Maliasili ina kesi Mahakamani baina yake na kampuni na watu binafsi ikidaiwa Sh.23,399,564,809 ukurasa wa 238. Kuna hatari ya kulipa fedha hizo kutoka kwenye bajeti endapo Wizara ya Maliasili na utalii itashindwa katika kesi hizo zilizoko Mahakamani.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara hii ni muhimu kwa ustawi wa utalii nchini katika taasisi za Serikali. Wizara hii ni kinara kwenye madeni makubwa kuliko taasisi yoyote, kiasi hicho ni zaidi ya fedha za bajeti ya maendeleo. Wizara hii imefanya matumizi ya Sh.3,559,102,398 na hajalipwa. Waziri akija kuhitimisha ajibu jambo hili likoje?

Mheshimiwa Naibu Spika, safari za ATCL kutochochea ukuaji wa utalii nchini. Uamuzi wa kufufua Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) ulipaswa kwenda sambamba na soko la utalii nchini. Kwa sababu Sekta ya Utalii ndiyo sekta kinara wa ongezeko la mapato ya kigeni na takwimu zinaonesha Kenya ndiyo inaongoza kuleta utalii nchini baada ya Marekani na tatu Burundi. Sasa jambo la kushangaza ATCL imetangaza kwa itaanza kufanya safari mara nne kwa wiki kutoka Dar es Salaam – Afrika Kusini. Ukiangalia masoko 15 yanayoongoza kuleta idadi kubwa ya watalii nchi ya Afrika Kusini ni ya nane. Sasa naomba Waziri akija kujibu anijibu yafuatayo:-

Je, kama hatuwezi kuitumia ATCL kuchochea soko la utalii tutaitumia kwa ajili ya kukuza sekta ipi? Napenda pia kujua uamuzi wa kupeleka ATCL Afrika Kusini baada ya kuanza na safari ambazo kuna soko kubwa la utalii, uamuzi huo unatokana na nini? Pia ni kwa namna gani ndege mpya ya ATCL mfano Dreamliner zinavyotumika kuchochea Sekta ya Utalii nchini? Napenda kujua kama upo mkakati kabambe wa kuyafuata masoko hayo ya utalii?

Mheshimiwa Naibu Spika, migogoro ya hifadhi na wananchi Mkoa wa Katavi; kuna migogoro inayoendelea katika Jimbo la Mpanda Vijijini, Kata za Vijiji vya Lyamgoloka, Iseganyanya, Isengule, Chamalendi, Ihefu, Kapalamsenga, Ikola, Karema. Wananchi hawa wanateswa na Askari wa Maliasili kwa maagizo kutoka kwa Mkuu wa Wilaya Mheshimiwa Mhando, wanapigwa risasi, wanachomewa nyumba na mifugo yao inatozwa faini kubwa. Sasa nataka kufahamu ni sheria gani inatumika kuwanyanyasa hawa raia wakati lengo la Serikali ni kutatua na si vinginevyo?