Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushuruku kwa kunipa nafsi hii. Naomba niungane na wenzangu kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Kigwangalla pamoja na Naibu wake Mheshimiwa Kanyasu, Katibu Mkuu na wafanyakazi wote wa Wizara ya Maliasili na Utalii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa naunga mkono hoja. Pia naomba niendelee kumshukuru Mheshimiwa Rais kwa kuweza kuruhusu baadhi ya maeneo ya wafugaji na wakulima waweze kupatiwa maeneo ya kulima na maeneo ya malisho.

Vilevile naomba niendelee kusema kwamba maeneo ya kilimo na malisho ya mifugo yameendelea kupungua kutokana na ongozeko kubwa na watu hivyo basi, unakuta eneo la kilimo halitoshi, lakini pia eneo la malisho ya mifugo haitoshi. Ombi langu, Serikali iweze kuridhia kupunguza eneo la hifadhi na maeneo ya akiba kurudi kwa wananchi ili waweze kupata maeneo ya kulima na maeneo ya kulishia mifugo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naiomba Serikali izingatie kauli ya Mheshimiwa Rais kwa kuweza kuendelea kutenga maeneo ya wafugaji na wakulima. Ukiangalia migogoro mingi iliyopo nchini ni kutokana na upungufu wa ardhi ya wananchi kulima lakini pia na malisho ya mifugo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kule kwetu Kasulu, Eneo la Akiba la Makere Kusini, bado kuna mgogoro mkubwa pamoja na kwamba Serikali imeongeza eneo kidogo, lakini bado wananchi wana mahitaji makubwa ya kupata eneo la kulima kwa sababu watu wameongezeka, ardhi inabaki kuwa ile ile naomba Serikali iweze kuruhusu kuongeza kipande kingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, niombe watu wa TFS waache kuwasumbua wananchi, waendelee kuwaelimisha, kwa sababu nimeshawahi kusimama hapa kulalamika kuhusu watu wa TFS wanavyowasumbua wananchi. Naomba wawaelimishe kwa kukubaliana na kuwaelekeza jinsi gani wanatakiwa kufanya kuliko kuchukua wakati mwingine mali zao, kuchukua pikipiki wakachoma, wakati mwingine kuchua baiskeli zao. Wawaelimishe, wakae nao wakubaliane ili wote waweze kutoka kwa pamoja.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Kengele imeshagonga Mheshimiwa, ahsante sana

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.