Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili nichangie hoja iliyopo mezani. Pia namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa uhai na wakati huo nawashukuru sana wananchi wa Urambo kwa kunipa ushirikiano wa hali ya juu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue nafasi hii kuwapongeza sana Mheshimiwa Waziri Dkt. Kigangwalla, Naibu Waziri Mheshimiwa Kanyasu, Wakuu wa Idara wote wa Misitu, Wanyamapori na kadhalika. Watendaji wote kwa kweli Wizara hii wanastahili sifa hongereni sana. Wameanza vizuri, tunawatakia kila la heri, waendelee na kazi kubwa wanayoifanya hadi wakati huu.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nichukue nafasi hii kushukuru ushirikiano ambao nimeshakuwa naupata na Wizara hiyo. Kwa mfano, alipokuwepo Naibu Waziri wakati huu Mheshimiwa Hasunga nilimwelezea kuhusu mgogoro wa mpaka nilionayo na tukaenda naye mpaka Urambo namshukuru sana. Aliiona, akajaribu kusuluhisha lakini baadaye akaondolewa kwenye Wizara hiyo. Kwa hiyo naamini waliopo watafuatilia huo mgogoro ambao nazungumzia kati ya wananchi na mipaka.

Mheshimiwa Naibu Spika, sijui kama wenzangu Waheshimiwa Wabunge kama wanajua Urambo nasi tuna game reserve, wanaongelea Ngorongoro lakini wasisahu na sisi Urambo tuna game reserve, kuna wanyamapori hawa wanaowaona huko nasi tunao, lakini pia tuna Hifadhi ya Msitu wa Ugalla.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kumekuwa na mgogoro wa mipaka kwa muda mrefu hasa katika Kata za Nsenda, Ukondamoyo, Ugalla na Uyumbu na hasa katika maeneo ya Lunyeta ambapo tulikwenda na Mheshimiwa Hasunga, Holongo, Utenge, Mwagimagi, Izengabatogwile, Magangi, Tebela na sehemu nyingi tu, chanzo chake ni nini?

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwaambie Wizara kwamba katika miaka 2007 Serikali ilirasimisha mipaka ya vijiji na wakaweka mawe ambayo yapo mpaka sasa. Baada ya kurasimisha mipaka Wizara ya Maliasili na Utalii nao wakaja na mipaka yao ambayo ikawarudisha nyuma kama kilometa 54 hivi na bahati mbaya wakachomewa nyumba na mali zao. Tukalileta hapa hapa wakati huo akiwa Mheshimiwa Pinda, Waziri Mkuu kwa sababu tume iliundwa na matokeo yake yakaonekana kweli wale wale wananchi walionewa. Wamechomewa mali zao, lakini walikuwa katika mipaka ambayo ni halali ambayo ipo mpaka sasa kwa kurudishwa nyuma. Tukawabembeleza wananchi wale tukasema suala hili litaendelea kushughulikiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, mipaka ile sasa ipo miwili, mpaka wa Serikali wa kwanza ambao ni wa halali kabisa na Mheshimiwa Hasunga aliiona. Wananchi wa kule wameendelea wanakuonesha mipaka kwa kufukua kwa mikono tu. Kwa hiyo kuna mipaka kwa kufufua kwa mikono tu kwa hiyo kuna mipaka ile ya zamani ipo na ni mipaka ya sasa hivi ambayo imewarudisha nyuma.

Mheshimiwa Naibu Spika, maana yake ni nini? Ni kwamba, sasa Serikali iende ikakae na wananchi ione, nami ningetoa wito kwa Serikali yenyewe kuwa ni Maliasili lakini waende na Ardhi kwa sababu wao ndio waliweka ile mipaka ya kwanza kabla Maliasili haijaja na mipaka ya pili. Kwa hiyo wananchi wanaomba waende wakaone na nitafurahi sana kama watafuatana na uongozi wa Wizara ya Ardhi ili wakaone kosa la wananchi nini, walikaa pale kihalali lakini wakawachomea mali zao.

Mheshimiwa Naibu Spika, Maliasili ilipokuja na mipaka ya pili ndio ikasababisha wale wananchi hawapo pale kihalali. Sasa wananchi wanauliza, je, mpo tayari kuwarudisha pale walipokuwa? Kwa sababu kwa kuwapunguzia kilomita nne sasa hivi hawana mahali pa kutosha pa kulima na walizoea mashamba yao na wafugaji pia hawana mahali pa kufugia. Kwa hiyo tunaomba sana Serikali iende kule.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, kuna tatizo…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)