Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Vedasto Edgar Ngombale Mwiru

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kilwa Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. VEDASTUS E. NGOMBALE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Nianze na kuwapongeza Mheshimiwa Kigwangwala na Mheshimiwa Kanyasu kwa kazi nzuri, hongereni sana mnakwenda vizuri. Mimi nianze na suala zima la utalii; kwa sababu ya kazi yenu nzuri, sasa tunazidi kupata watalii wengi lakini kuna maeneo ambayo huko mwanzo walikuwa wanapatikana watalii wengi lakini sasa watalii wamepungua. Kwa mfano ukisoma ukurasa wa 94 katika lile jedwali la vyanzo vya kale katika sehemu za Kilwa mwaka 2014, 2015 watalii walifikia mpaka 2700 lakini sasa hivi watalii wamepungua. Sasa hii inaonesha namna gani ambavyo Wizara bado haijajizatiti katika kuendeleza utalii hususan katika eneo la mikoa ya Kusini.

Mheshimiwa Naibu Spika, chanzo kilichotajwa pale ni kimoja tu ilhali sisi tunavyo vyanzo vingi. Kwa mfano tuna chanzo cha Pango la Nang’oma ni pango kubwa tu lakini pale sijaona kama kimefanyiwa chochote. Kutokana na hilo kwa sisi watu wa kusini bado inaonekana neno utalii kwetu ni msamiati, na ni msamiati ambao tafsiri yake hujajua maana yake. Kwahiyo naomba Wizara ijaribu kutoa elimu kwa wananchi ili waweze kuona namna gani wanajihusisha kwenye utalii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini lingine ambalo ningependa kusema, niwapongeze kwa kutoa ruhusa sasa ya kufanya ule uwindaji wa wenyeji, sasa wenyeweji wanaweza wakanufaika maana sasa wanyama wamekuwa wengi na sisi tumezikaribia mbuga zile lakini hatupati chochote; kwa hiyo kwa ruhusa hii itawasaidia sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuna changamoto moja. Mwaka 2014 kama sikosei kulikuwa na operesheni ile ya Tokomeza ambayo ilisababisha kunyang’anya zile silaha za wenyeji; silaha zote zilinyang’anywa na mpaka sasa hivi ninavyozungumza zile silaha bado hazijarudishwa. Sasa kama mmeruhusu silaha walizokuwa wanamiliki wenyeji kihalali bado mnazo ninyi hilo nafikiri nalo litakuwa tatizo. Nomba Wizara ishughulikie ili warudishiwe zile silaha ili na wao waweze kunufaika kuwinda katika maeneo haya ya wazi kama eneo la Kilwa na sehemu nyingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ni kuhusu tembo. Tembo wameongezeka sana, na sisi ambayo majimbo yetu yanapakana na Selou imekuwa shida. Ukitaka kwenda baadhi ya vijiji ni lazima ule-timing kwamba sasa hivi huwezi kupita sasa hivi unaweza kupita. Kule kwangu katika Kijiji cha Mkarango tembo ameshawahi kuua mtu katika kipindi cha miezi miwili iliyopita.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo mimi naomba Wizara ijaribu kuwa na connection nzuri na watu wale wa maliasili ili yanapotokea haya matatizo tunapotoa taarifa kwenu haraka sana waje ili waweze kuwarudisha tembo, vinginevyo basi muangalie njia nyingine ambao zinaweza kusaidia kudhibiti hawa tembo; tembo wamekuwa wengine sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ni suala zima la ustawi wa watu wa kusini ambao wanakaribiana na vyanzo na vivutio vya utalii na hususan sisi ambao tunakaribia Pori la Akiba la Selou. Niseme tu kwamba labda Wizara iangalie upya namna ya uwekezaji wa rasilimali hizi za utalii. Sisi kule kusini tuna pori tuna Mji wa Kale wa Kilwa na vivutio vingi lakini mpaka sasa hatuna chochote, yaani hakuna yale manufaa ya moja kwa moja. Kama chuo hatuna hata chuo kimoja cha utalii; basi Wizara angalieni namna ambavyo sisi tunaweza tukanufaika moja kwa moja, maana ukikaribia waridi basi na wewe unukie.

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi ni kama tumekuwa watunzaji tu wa yale mapori; na ndiyo maana utalii kwetu kimekuwa ni kitu cha mbali sana. Kwa hiyo Wizara hebu jaribuni kutengeneza kitu ambacho kitakuwa motisha kwa watu wa kusini na wao waukaribie utalii hiyo itatusaidia sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine naomba Serikali ishughulikie mgogoro kati ya Vijiji vya pale Zinga Kibaoni. Kuna Kijiji cha Ngarambi, Kijiji cha Mtepela na Kijiji cha Namatewa na Hifadhi ya Selou bado kuna migogoro.

Mheshimiwa Naibu Spika, na la mwisho kabisa ninaomba sasa basi hili wenzangu wengi wamelifanya, watu kama kina Samata watumike vizuri ili basi utalii uweze kwenda…(Makofi)

(Hapa kengele ililiakuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)