Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru, kwanza nitoe pole kwa shule ya Wasichana ya Ashira Mabweni yao yameungua moto jana na wanafunzi zaidi ya 100 hawako kwenye hali nzuri na eneo hili linapakana na Mlima Kilimanjaro kwa hiyo, niombe na TANAPA pia waweze kuangalia ni namna gani tunaweza tukashirikiana katika kurudisha hadhi ya shule yetu ya Ashira ili iweze kuwa kwenye hali nzuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nitoe pongezi kwa TANAPA kwa kazi nzuri wanayoifanya na ujirani mwema wa vijiji 88 vya Mkoa wa Kilimanjaro kupitia KINAPA wamefanyakazi nzuri na wameshirikiana na Vunjo development foundation (VDF) pamoja na Ofisi ya Mbunge tumeweza kutengeneza barabara zaidi ya kilometa tisa kwa hivyo niwapongeze sana TANAPA kupitia Mkurugenzi wake Kijazi na Mwenyekiti wa Bodi Gen. Waitara na wote pamoja na Sakayo Mosha sekondari imejengwa vizuri, Zahanati ya Kitoo wanafanyakazi nzuri na mtu akifanyakazi nzuri yapasa kumpongeza, tunawapongeza sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na tabia yetu sisi Watanzania kwenye sekta ya utalii badala ya kuuza utalii au kuuza huduma tunauza neno “samahani”. Huduma vigezo vyetu au uwezo wetu wa kutoa huduma unavyokuwa chini badala ya kuona namna gani ya kuboresha kutoa viwe kwenye standard tunatoa neno “samahani” hasa kwenye mahoteli yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitasema kwanini nasema hivyo; kwanza sekta ya utalii ndiyo sekta kuu inayoongeza fedha za kigeni hapa Nchini. Asilimia 25 ya forex yote inatokana na utalii sasa tusiangalie ugali wa leo tu, nitumie lugha rahisi, tuangalie kesho. Nasema hivyo kwa sababu ukiangalia bajeti ya Wizara hii ni bilioni 120, fedha za maendeleo ni bilioni moja tu za ndani za nje ni bilioni 47.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ukiangalia maduhuli na mwaka jana niliomba tena, ukiangalia maduhuli yanayotokana kwa mfano na TANAPA peke yake mwaka jana ilikuwa zaidi ya bilioni 292. Unamlisha Ng’ombe vizuri ili umkamue vizuri na aweze kukuletea tija zaidi. sasa kwa kweli bajeti ya Wizara hii ni kidogo sana. Kwa mfano, Bosi ya utalii, Jaji Thomas Mihayo ambaye ni Mwenyekiti na wenzake wanafanyakazi nzuri lakini tunawawezesha kiasi gani waweze wakatangaza utalii wetu? Fedha zinazotolewa kwenye kutangaza utalii, kwa mfano, tukijifunza kwa wenzetu wa Kenya ni zaidi ya Dola milioni 100 yaani zaidi ya bilioni 200 yaani fedha zote za bajeti ya Wizara hii hazitoshelezi kuutangaza utalii.

Mheshimiwa Naibu Spika, pengine nipendekeze tu; maduhuli yanayotokana na Wizara hii Serikali ione umuhimu wa kuacha ndani ya Wizara angalau kwa miaka mitano ili Wizara iweze ikakua na GDP yake iweze ikakua ili Taifa liweze likavuna zaidi kutokana na hali ya namna hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, viko vigezo vingi ambavyo vinarudisha nyuma utalii wetu. Kwa mfano, work permit za expert kama kuna wafanyakazi 100, wafanyakazi wawili ambao ni experts au wataalam kwanini wasipewe mazingira rafiki ya kuweza kufanyakazi vizuri. Ubora wa vyakula vyetu, kwa mfano, lile katazo la vyakula vya mifugo au maziwa kutoka Kenya, kodi nyingi nyingi tuangalie ushindani zaidi kwenye standardization, standards zetu tuziboreshe zaidi ziashindane badala ya kuwelka restrictions ambazo siyo rafiki, utitiri wa kodi. Nipongeze Kambi ya Upinzani wameandika vizuri utitiri wa kodi uliopo, Kamati nayo imeandika vizuri pia, tuangalie utitiri mwingi sana kwenye kodi katika Wizara hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna matamkao yanayotolewa, Serikali ikitoa matamkoa iangalie sana. Kwa mfano, matamko ya magonjwa kama ya Dengue ambayo watalii wanaibebaje kwamba Tanzania tayari yote ina magonjwa ya namna hiyo wanaogopa hata kuja Tanzania. Hata hii mifuko ya plastic namna gani wanafanya package, restrictions ziko namna gani, tamko la Serikali liko namna gani kwa hivyo matamko haya tunayoyatoa lazima yaangalie kwa mapana yake, utalii Kusini na mazingira, UNESCO wako kwenye position gani tunaitangaza namna gani Dunia kwenye mambo ya namna hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nasema hivyo kwa sababu ukiamua kupanga vizuri, kwa mfano, Kilimanjaro marathon wakati wa low season ukaipanga kama ni package moja ya kuanzia unawaambia watalii wanakuja wanaanzia Arusha kwenye kuangalia wanyama Serengeti, wanakuja kwenye Kilimanjaro marathon, wanatoka kwenye Kilimanjaro marathon kwenye kukimbia huko wanakwenda Zanzibar (Zanzibar music festival) kwenye raha huko, wanakuja Dar es salaam, Dar es salaam wanaangalia biashara na Mji ulivyo, wanakwenda mbuga za Saadani-Bagamoyo kwahivyo inakuwa ni package moja na ukiipanga vizuri ni taaluma tu yaani inakuwa ni tourist plan ambayo ikiipanga as a tour moja faida yake ni kubwa kwa Taifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hivyo, wataalam wapo, tuwawezeshe watalaam wetu waweze kuzifanya hizi tour zikaweza kuwa na hii route ikawa na manufaa na maslahi mapana kwa Taifa. Kwa mfano, kipindi cha low season, kwa mfano, Easter time ukasema wiki mbili nzima ni za plan nzima ambayo ina-compensate sio ina compensate ile zitakwenda sambamba na high season, ukimaliza kipindi cha Easter high season nayo inakuja kwa hivyo unakuta mwaka mzima utalii na tuweke priority kutokana na vivutio vyetu vya utalii. Kipaumbele kwenye eneo hili kwa ukubwa wake kiko hivi, kipaumbele kwenye eneo hili kiko hivi, eneo hili la kutangaza vivutio vile tulivyonavyo yaani kwa lugha nyingine niseme we must organize what we have and plan for it, tu-plan, tu- organize, turatibu, tuweze kuelekeza na kuweza kutawala vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia watu kwa mfano, European wana-route zao wanazi-plan vizuri unaanzia Belgium, unakwenda France, unakwenda Spain, unakwenda Germany wanakuwa ni package moja sasa hapa kwetu na vivutio vingi hivi tulivyonavyo vya utalii yata-stick big. Mheshimiwa Waziri naujua uwezo wako na mmetulia vizuri sana kwenye Wizara sasa hivi nikupongeze kwa hilo na ubinifu washirikishe wadau walio wengi, tuishirikishe Dunia, tushirikishe wawekezaji kwenye sekta hizi kwa sababu uwekezaji kwenye utalii pamoja na communication kwenye utalii ni watoto pacha, wanarandana, wanaingiliana sasa namna gani unachukua wataalam hawa, kwa mfano, Makampuni ya humu ndani tukatumia…

Mheshimiwa Naibu Spika, dakika moja namalizia sekunde 30; Makamouni ya huku ndani yakatmika vizuri katika kuwekeza na kutangaza utalii badala ya Makapuni ya humu ndani kutumika na watu wa nje zaidi tuyawezeshe Makapuni ya ndani na wao waweze kuwekeza vizuri katika sekta hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana Mwenyezi Mungu akubariki.