Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Dr. Immaculate Sware Semesi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana niweze kuchangia katika Wizara hii muhimu sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitajikita katika sekta ya misitu kwa sababu sekta hii ni muhimu sana kwa uhai wetu na kwa uhai wa Nchi yetu kwa masuala ya kijamii pamoja na kiuchumi.

Mheshimiwa Naibu Spika, hali yetu kuhusu suala la misitu iko bado tete sana kwa sababu zaidi ya asilimia 90 ya nchini kwetu tunategemea bidhaa zinazotokana na misitu hususani kwa shughuli za Nishati aidha kwa kutumia kuni au shughuli za mikaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile tuna suala zima la Sheria ambazo zinaangalia sekta hii kwa ujumla ambazo zinajikanganya inavyoshughulikia misitu yetu. Tuna Sheria mbalimbali mfano, The Local Government Finance Act na Mining act nafikiri mwaka jana tulifanya marekebisho katika Mining Act na Finance Act kwenye masuala ya uvunaji wa chumvi katika maeneo hususani ya mwambao.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kule maeneo ya mwambao tuna misitu mahususi sana, misitu ya mikoko. Sasa baada ya kufuta taratibu ambazo zinashughulikiana na mazingira, watumiaji au mining katika maemeo haya imekuwa kubwa sana na mikoko hii imekuwa ikikatwa kwa kasi sana na misitu hii ni muhimu sana katika utunzaji wa mazingira na inasaidia kutu-shield na zile dhoruba za baharini. Sasa tunapozidi kuikata hii miti tunazidi kujiweka katika mazingira hatarishi pale tunapopata dhoruba kama wenzetu wa Mozambique hiki kimbunga kilichopita kwa bahari nzuri hakikutupata ilihali ingetupata basi madhara yake yangekuwa makubwa sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile Sheria yetu ya Mipango Miji ya mwaka 1982 inakataza shughuli za kilimo na upandaji wa miti kwa ujumla wake katika maeneo ya miji. Sasa nafikiri Sheria hii iangaliwe upya kwasababu unapokuwa na miti au misitu tunasema maeneo ya Miji tunasema ni mapori lazima yaondolewe. Lazima tuliangalie hili kwa ukubwa wake na mapana yake na effect ambazo zinaweza zikajitokeza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nigusie suala la biashara la soko la mbao Nchini; biashara hii inaweza ikatuinua kiuchumi, tunaongelea mabilioni ya Dola za Kimarekani katika biashara hii lakini biashara hii kwa sasa hivi imekuwa kama biashara haramu ambapo tunavuna sana kuliko kuangalia uvunaji endelevu na jinsi soko hili linavyotakiwa kufanya kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba suala la biashara la soko la mbao Nchini liangaliwe na pia tuweze kuviendeleza viwanda vyetu vya ndani vya kutumia mbao viweze kutumia mbao yenyewe kama mbao hata zile by product nazo ziweze kuzalisha na kuleta manufaa kiuchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nigusie suala la TFS; TFS sasa hivi ni kama agency. Naomba kulia mkazo kwamba sasa igeuke kuwa regulatory authority najua mchakato unaendelea basi naomba ufanywe kwa haraka ili TFS iweze kusimamia masuala yote ya mazingira na miti maeneo ya mijini, vijijini, halmashauri wawe na authority ya kuweza ku- regulate na siyo kuingilia Sheria na Sera mbalimbali ambazo zinawakwaza wao sasa hivi kutekelza majukumu yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuangalia umuhimu wa misitu Nchini na Nchi zinazotuzunguka, Tanzania imeingia maridhiano na makubaliano mbalimbali ya Kimataifa basi naomba Tanzana sasa ijikite na iwe reflected kwenye bajeti na watupe update. Kwa mfano, hapa hapa Nchini tumeingia mkataba wa Zanzibar declaration status iko wapi hususani katika soko la biashara ya mbao, African forest scape restoration borne challenge na UN-CCD sasa Tazania imesimama vipi ili kuweza kuboresha hali ya miwitu yetu Nchini? Tunaomba Mheshimiwa Waziri anapohitimisha basi atupe status yetu ikoje au kuna vikwazo gani ili Bunge hili liweze kusaidia kuweka mambo vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia naomba nigusie status ya Community base forest management; najua kuna policy mahali sijui imeishia wapi sasa uharibifu mkubwa wa mazingira haya ya misitu yanatokea katika vijiji vyetu. Vijiji tumevipa mamlaka, naomba Serikali husika, Wizara husika iangalie masuala ya Vijiji vinasimamiaje misitu ili viwe endelevu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. (Makofi)