Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, nawapongeza Mheshimiwa Waziri na Naibu wake, Makatibu Wakuu na timu yote.

Mheshimiwa Spika, nilishaongea juu ya josho eneo la Linga (Keta), suala la samaki wadogo (vituwi) lifanyiwe utafiti ili Wananchi wanufaike na samako hao, kuboresha mialo, mazingira ya uvuvi, pamoja na umuhimu wa boti.

Mheshimiwa Spika, ukopeshaji/ruzuku ya engine za boti isiwe lazima kwa vikundi kwani katika vikundi wakati mwingine uwajibikaji huwa ni dogo.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, hata kama atanunua mmoja bado hawezi kuvua pake yake na ajira zitakuwa nyingi na uvuvi utaimarika. Ubinafsi ndiyo zana kuu ya kumhamasisha mjasiriamali, ‘kwamba ninanufaika vipi?’

Mheshimiwa Spika, nawasilisha.