Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, nianze na kumpongeza Mheshimiwa Waziro Mpina, Naibu Waziri Mheshimiwa Ulega, Makatibu Wakuu na Watendaji wa Wizara ya Mifugo kwa hotuba yao nzuri ya bajeti iliyowasirishwa hapa Bungeni.

Mheshimiwa Spika, naomba na mimi nitoe mchango wangu kwa mambo yafuatayo;

Mheshimiwa Spika, Makusanyo ya Maduhuli. Niipongeze Wizara kwa juhudi kubwa sana ya ukusanyaji maduhuli ya zaidi ya asilimia 183. Hii imeonesha jinsi mlivyo makini sana. Yapo malalamiko kwa baadhi ya wavuvi ambao wamekuwa wakilalamikia watendaji wa Wizara kuwatoza faini kama kuna kosa lakini risiti wanayopatiwa inaandikwa kiwango kidogo cha fedha. Je, Serikali inatambua hilo? na je, hatua gani zinachukuliwa kwa watendaji kama hawa wanaoiibia Serikali na kuwanyanyasa wafugaji na wavuvi?

Mheshimiwa Spika, kuna baadhi ya Halmashauri watendaji wa Serikali wamekuwa wakiwanyanyasa wafugaji. Je, Wizara imejipangaje kuona utaratibu wa sheria na kanuni zinafuatwa kumlinda mfugaji?

Mheshimiwa Spika, Maeneo ya Malisho na Migogoro ya Wafugaji. Serikali inaweka mkakati gani wa kuhakikisha inamaliza mgongano wa wafugaji baina ya wakulima na dhidi ya hifadhi za taifa kutokana na upungufu wa maeneo ya malisho?

Mheshimiwa Spika, wafugaji wamekuwa wakinyang’anywa mifugo yao na askari wa wanyamapori na kusababisha unyanyasaji mkubwa sana na wananchi kufilisiwa. Je, huwa wanatumia sheria gani?

Mheshimiwa Spika, Kuimarisha Sekta ya Maziwa. Serikali imejipangaje kusaidia viwanda vya maziwa nchini kwa kuondoa tozo nyingi? (ukurasa wa 28) kulinda viwanda vyetu na kuvutia wawekezaji wa nje na ndani ikiwa ni pamoja na kuongeza ajira nchini.

Mheshimiwa Spika, pia changamoto nyingine ni wingi wa taasisi za kudhibiti na ukaguzi zipatazo 11 ikiwa ni pamoja na kutoza kila flavor katika maziwa.

Mheshimiwa Spika, ningeomba Serikali itupatie mkakati wa kukuza sekta hii ya maziwa. Naunga mkono hoja.