Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Spika, nawapongeza wote ndani ya Wizara katika utendaji wao wa kazi nzito kutokana na wengi wao ambao ni wafugaji na wavuvi ni wananchi wa kawaida, ambao wanahitaji kupewa elimu ya kuwawezesha kufanya shughuli zao kwa ufanisi na tija kwa mapato yao. Hivyo hazina waone umuhimu wa kuongeza ukomo wa bajeti na fungu la miradi ya maendeleo kuweza kutolewa kwa ukamilifu.

Mheshimiwa Spika, napenda kuona umuhimu wa vikundi vya akina mama wanaojikita kwenye ufugaji wa kuku kama miradi ya kuwapatia uchumi kwa kupambana na umasikini. Akina mama wamekuwa na uwezo mdogo wa kufuatilia vifaranga na utunzaji wa vifaranga hivyo hadi kufikia kutoa mazao tarajiwa ya mayai au nyama, kuwa na gharama kubwa. Tunaomba Wizara/Serikali kuona utaratibu bora wa kuboresha utunzaji wa kuku wa kienyeji ili kuweza kuzalisha mayai na kutoa nyama kwa mahitaji makubwa kwa wananchi wetu, na kwa kuwa hawana gharama kubwa na wanastahimili madhara stahili kwa wastani mkubwa sana.

Mheshimiwa Spika, wafugaji wamekuwa wanasafiri sana maeneo mbalimbali ili kutafuta malisho. Hivi kwanini Serikali isiweke utaratibu wa mashamba ya malisho na yakafahamika na kuwaelimisha wafugaji kulima mashamba hayo kwa idadi ya mifugo yao? Pia tuone utaratibu wa kuboresha mifugo ya asili kulika kupandikiza wa kutupatia mifugo chotara na kusababisha kupotea kwa mbegu ya asili ya mifugo yetu.

Mheshimiwa Spika, jitihaa ya Wizara kutuwezesha kupata samaki wakubwa na wenye tija wa kuwapatia mapato ya kutosha wananchi wetu. Kikubwa tutoe elimu kwa wahusika na uvuvi na ufugaji kwa maendeleo na kukuza uvuvi na ufugaji bora nchini.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.