Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Zainab Mndolwa Amir

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. ZAINAB M. AMIRI: Mheshimiwa Spika, awali ya yote nimpongeze Waziri na Naibu Waziri kwa kazi kubwa wanayoifanya kwenye Wizara hii katika kusimamia majukumu yao ya kila siku ili kuhakikisha masuala yahusuyo mifugo na uvuvi yanatekelezwa.

Mheshimiwa Spika, Maoni; fedha zinazotengwa katika Wizara hii hazitoshi kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo. Naishauri Serikali itenge fedha za kutosha na pia fedha hizo zitolewe kwa wakati ili miradi iliyopangwa iweze kutekelezeka.

Mheshimiwa Spika, naishauri Serikali kuondoa gharama za leseni katika vyombo vya uvuvi kama ilivyo katika trekta. Naishauri Serikali kutokana na wingi wa ngozi zinazotokana mara baada ya kuchinja mifugo yetu kwa ajili ya nyama. Vijengwe viwanda vya kutosha hapa nchini mwetu vya uchakataji wa ngozi ili kuweza kupata ajira pia kuongeza Pata la Taifa.

Mheshimiwa Spika, naishauri Serikali iboreshe majosho yote nchini kwa ajili ya mifugo; na majosho hayo yatumike kwa mifugo tu na si shughuli zingine za kibinadamu. Naishauri Serikali itenge maeneo maalum ya malisho ya mifugo mifugo ili kuondoa kabisa migogoro iliyopo sasa baina ya wakulima na wafugaji ya kugombania maeneo kwa ajili ya kilimo kwa wakulima na kwa ajili ya malisho kwa wafugaji.

Mheshimiwa Spika, naishauri Serikali kuzingatia sheria na kanuni zilizopo pindi mifugo ikikamatwa. Kuna baadhi ya watendaji wa Wizara hawafuati sheria na taratibu zilizopo; hutaifisha mifugo hiyo ambapo ni kinyume cha sheria na kuanza kuipiga mnada na hivyo kuendelea kuleta mahusiano mabaya baina ya watendaji na wafugaji.

Mheshimiwa Spika, naishauri Serikali ipunguze tozo katika maziwa. Kwa mfano katika usindikaji wa maziwa, ladha ya maziwa, vifungashio na leseni za usafiri. Naishauri Serikali Ranchi zote walizopewa wawekezaji na kushindwa kuziendeleza zirudishwe Serikalini ili Serikali iweze kuziendeleza kwa kuziboresha na hatimaye zitumike kama maeneo ya malisho kwa wafugaji waishio pembezoni mwa ranchi hizo. Pia ranchi hizo zitumike kama shamba darasa kwa wafugaji wetu ili kuepuka kutohamahama kwenda kutafuta malisho.

Mheshimiwa Spika, naishauri Serikali iboreshe vyombo vya uvuvi katika bahari kuu. Pia kuwepo na meli kubwa za uvuvi. Ili viwanda viweze kupata malighafi za kutosha pia itapunguza uingizwaji wa samaki kutoka nje ambapo wakati mwingine samaki hao si bora kwa mlaji au kwa matumizi ya binadamu.

Mheshimiwa Spika, pia naishauri Serikali ijenge viwanda vya kuchakata samaki katika mikoa iliyopo pembezoni mwa Bahari ya Hindi.

Mheshimiwa Spika, mwisho nawatakia Waziri na Naibu Waziri afya njema na umri mrefu katika kuyatekeleza majukumu yao ya kila siku.