Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Spika, naomba nichangie hoja hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ufugaji wa samaki; kwa kuwa kuna umuhimu sana wa wananchi kupata lishe ya samaki ambapo samaki hawana madhara kama nyama, naiomba Serikali itoe elimu kwa wananchi namna ya kufuga samaki. Pia samaki hao watawapatia wananchi kipato.

Mheshimiwa Spika, nyavu za uvuvi kumekuwa na uchomaji wa nyavu holela kwa wavuvi. Hii siyo sawa, naomba kuishauri Serikali nyavu zinazochomwa basi zirudi kiwandani zikarekebishwe.

Mheshimiwa Spika, wataalam; kwa kuwa sekta ya ufugaji na uvuvi haina wataalam wa kutosha, naomba Serikali iajiri wataalam wa kutosha.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.