Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Muhammed Amour Muhammed

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Bumbwini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. MUHAMMED AMOUR MUHAMMED: Mheshimiwa Spika, Awali ya yote inapenda kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema kwa kutupatia uhai na uzima na kuwa tunaendelea na harakati zetu kama kawaida. Pia kwa namna ya pekee napenda kukushukuru wewe binafsi kwa kunipatia fursa hii ya kuchangia mada iliyopo hewani. Katika mchango wangu naomba nizungumzie mambo yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, kupigwa nyavu moto, Wavuvi kunyang’anywa zana zao za uvuvi na kupigwa Wavuvi na JWTZ; kumekuwa na utaratibu kwa kipindi kirefu, wavuvi wetu kunyang’anywa nyavu zao na kutiwa moto. Ni vyema watu hawa wakapelekwa Mahakamani, Mahakama ikaamua kuliko kuamuliwa maamuzi ya aina kama hii.

Mheshimiwa Spika, niongee vipigo wanavyopata Wavuvi; kumekuwa na utaratibu mbaya sana wa kupiga wavuvi kwa visingizio mbalimbali. JWTZ Kitengo cha Navy kimekuwa kikipiga wavuvi, hatari sana kabisa inatisha, inaumiza lakini pia inasikitisha sana.

Mheshimiwa Spika, niombe kwa heshima zote, Serikali ione umuhimu wa kutatua hili kwani linazidi kuleta changamoto kwa wavuvi na kwa Taifa kwa ujumla wake.

Mheshimiwa Spika, niendelee kuchangia kuhusiana na kunyang’anya wavuvi zana zao; kumekuwa na tatizo hili kwa kipindi kirefu sana, wavuvi wetu wamekuwa wakinyang’anywa zana zao kama nyavu, mashine, mitungi ya gesi. Kwa nini baada ya kunyang’anywa vifaa hivyo hawapelekwi kwenye sheria Mahakamani, matokeo yake vifaa hivyo vinabaki kwa wale waliokamata hadi lini? Tunaweza kusema wananyang’anywa na hawapewi vifaa vyao?

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.