Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. ANGELINE S. L. MABULA: Mheshimiwa Spika, nianze kwa kuunga mkono hoja. Pili, niwapongeze Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri pamoja na Watendaji wote wa Wizara kwa kazi nzuri wanayoifanya. Wamebadili sana hali ya utendaji kwa watumishi waliokuwa wanafanya kazi kwa mazoea.

Mheshimiwa Spika, haja yangu, Mheshimiwa Waziri naomba kufahamu mpango wa Wizara juu ya eneo la mafunzo kwa vijana wanaosoma Chuo cha Ngozi, Mwanza. Kiwanda cha Ngozi ambacho kilikuwa kinachukua wanafunzi na kuwapa mafunzo katika Kiwanda cha Ngozi maarufu kama Mwana Tanneries. Niombe kiwanda hiki kifufuliwe upya, mwekezaji apatikane ili tuongeze ajira kwa vijana wetu.

Mheshimiwa Spika, pili, nimepokea malalamiko toka kwa wananchi wakilalamikia wafanyabiashara toka nje ya nchi wanaingia moja kwa moja viwandani na maeneo ya uvuvi ili kununua bidhaa ya samaki badala ya kununua katika soko la Mwaloni, soko ambalo liko rasmi kwa biashara ya mazao ya samaki katika Ziwa Victoria.

Mheshimiwa Spika, tatu, niombe Idara ya Uvuvi wafike Jimboni kutoa elimu ya ufugaji samaki wa vizimba, ukizingatia kuwa zaidi ya 80% ya eneo katika Jimbo ni eneo la maji. Naomba tutumie maeneo ya fukwe za ziwa ambayo hayatumiki kama beach yatumike kufanya ufugaji wa vizimba (cape fishing).

Mheshimiwa Spika, nne, tunao vijana katika vikundi vya ufugaji walipata mafunzo ya awali ya ufugaji kuku, sungura na kadhalika. Niombe Wizara iwezeshe katika kuwapa mtaji ikiwemo vitendea kazi na namna bora ya ujenzi wa mabanda ya sungura, kuku na kadhalika yenye kuzingatia viwango vinavyokubalika.

Mheshimiwa Spika, tano, kuna Chama cha Ushirika cha Wavuvi ambao wameshajiunga wanasubiri uzinduzi rasmi. Niombe Mheshimiwa Waziri awazindulie ili kufungua milango kwa wafanyabiashara wengine wa samaki na wafugaji pia.

Mheshimiwa Spika, sita, ombi maalum; naomba vifaa vya uvuvi ili kuwezesha vijana waliopo katika sekta hii ya uvuvi wavue kwa tija.