Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja kwa mchango ufuatao:-

Mheshimiwa Spika, mifugo itasaidia Watanzania zaidi iwapo uchumi wa viwanda utashika kasi. Cha kushangaza ni kuwa hata viwanda vilivyopo sasa havitumiki kabisa. Nikitolea mfano, Kiwanda cha Nyama cha SAAFI kilichopo Sumbawanga kinasemekana ni miongoni mwa viwanda bora kabisa vya nyama, lakini baada ya uwezo wa mwekezaji mzawa kutetereka Serikali imeshindwa kabisa kuweka mipango ya kukiendeleza, badala yake ng’ombe wanasafirishwa toka Sumbawanga mpaka Dar-es-Salaam na wakati mwingine ng’ombe hupelekwa Zambia kwenye viwanda vya nyama.

Mheshimiwa Spika, naishauri Wizara ione namna ya kukitumia kiwanda hiki. Nilipata nafasi ya kutembelea kiwanda, ni kiwanda kizuri kina miundombinu ya kisasa mingi inayowezesha mifugo wote na masalia yake yote kuongezewa thamani, ikiwemo damu, ngozi, kwato, mifupa na kadhalika. Serikali iliweza kutaka kushirikiana na mwekezaji ili aweze pia kulipa deni la Serikali na kutafuta masoko duniani. Masoko ya nyama yalipatikana sehemu mbalimbali ikiwemo Comoro, Shelisheli, Uarabuni na kadhalika, hata hivyo Serikali imekaa kimya bila kutoa uamuzi. Naomba watusaidie kiwanda kile kikifanya kazi ng’ombe wa wafugaji wa Rukwa, Katavi, wangepata soko na kuvutia ufugaji. Naomba sana Serikali isaidie kiwanda hiki kipate mtaji wa kazi na ikiwezekana isimamie yenyewe na mwekezaji yuko tayari sasa PPP na Sera ya Viwanda tunaitekeleza kweli namna hii.

Mheshimiwa Spika, wavuvi wananyanyasika kupita kiasi; Maafisa hawajengi mahusiano baina yao na wavuvi, mahusiano ni ya paka na panya. Nashauri Serikali ifanye mabadiliko katika kusimamia sekta ya uvuvi iwe rafiki kwa wadau wote.