Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. TUNZA I. MALAPO:Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi nichangie katika Wizara hii ya Elimu, mimi nitajikita zaidi kwenye vyuo vya ualimu kwa sababu nina experience huko.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vyuo vya ualimu wamebadilisha mtaala kwa mfano chuo ambacho kilikuwa kinafundisha diploma ya ualimu wa ngazi ya sekondari unakuta sasa hivi kimepangiwa diploma katika ngazi ya elimu ya awali. Mtaala huo umebadilishwa sijui kwa vigezo vipi, sijui kwa tafiti zipi sasa mbaya zaidi mtaala umebadilishwa, wakufunzi hawajui nini wanachotakiwa kufundisha, mtu anapewa kozi pale mwezi mmoja ama miwili unatafuta material hujui uanzie wapi, hakuna kitabu, hakuna rejea na kama rejea zipo zimeandikwa kwa lugha ya kiingereza lakini wale watoto tunatakiwa tufundishe kwa lugha ya kiswahili; shida sio kutafsiri lakini ipi ni tafsiri sahihi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumekuwa tukichezea elimu utafikiri ni kitu ambacho hakina msingi. Sera ya Elimu inasema elimu bure, Sera ya mwaka 2014 tumekubali elimu bure maana yake ni nini? Serikali inajinasibu wanafunzi wengi wanasajiliwa shuleni, shule za msingi lakini nataka niwaambie jambo la kusikitisha Mheshimiwa Ndalichako pita kwenye vyuo vya ualimu, nenda kaangalie capacity ya chuo ni wanafunzi 450 unakuta waliosajiliwa ni wanachuo 50; maana yake ni nini? Baada ya muda wanafunzi wale wa shule za msingi wataongezeka kuwa wengi lakini walimu hakuna, tunatengeneza kitu gani? Tusifanye vitu kwa siasa wakati tunaongezea wanafunzi pia tuhakikishe walimu idadi yao inaongezeka. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi naongea kwa ushahidi nenda Chuo cha Ualimu Mtwara Kawaida kaangalie capacity ya chuo na kaangalie wanafunzi misuse of resources.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara inaitwa Wizara ya Elimu, Teknolojia na huko inaendelea. Jambo la kusikitisha sana tunapoenda kwenye vyuo vya ualimu mtandao wa internet hakuna wa uhakika, maana yake mwalimu huyo hana vitabu vya uhakika, mtandao wa internet hakuna na kulikuwepo na programu inaitwa ICT implementation in teacher education.
Mheshimiwa Waziri unapokuja kuhitimisha naomba nipate ufafanuzi programu ile imefikia wapi, ukienda kwenye vyuo vya ualimu utakuta kuna kompyuta nyingi ni mbovu, mtandao wa internet hakuna kabisa, naongea kwa ushahidi, walimu wale mnataka wafanye kitu gani? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapozungumzia elimu hatuwezi kumuacha mwalimu. Wakufunzi wa vyuo vya ualimu na vyuo vya ualimu kwa ujumla wake vimeingia kwenye mfumo wa NACTE ingawa mimi sijui na sioni utekelezaji wake,
lakini mfumo ule wa NACTE una stahiki zake lakini mpaka leo tunapoongea baadhi ya wakufunzi wa vyuo vya ualimu wanalipwa kwa stahiki za Wizara ya Elimu, wanafanya kazi mpaka muda wa ziada kwa sababu ule mfumo una mambo yake, mwisho wa siku mtu analipwa kama bado anahudumiwa na Wizara ya Elimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tunataka ufafanuzi wale watu wapo katika mlengo gani, kama mmeamua kuwapeleka NACTE wapelekeni NACTE na stahiki zao zote na kama mnaamua wabakie Wizara ya Elimu basi wabakie na stahiki zao zote. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza vyuo vya ualimu ni vichache siji tatizo ni nini, mnashindwa kukaa mkajua mahitaji ya wakufunzi mnashindwa kuboresha miundombinu, ukienda kwenye Chuo cha Ualimu Mtwara Kawaida nakiongelea kwa experience, mabwenini kule hali ni mbaya, unamfundisha nini mwalimu? Hali ni mbaya, miundombinu mibovu, madarasa yapo hayaeleweki yaani ule utanashati wa mwalimu unapotea. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri atakapokuja atueleze kwenye vyuo vyote vya ualimu kulikuwa na shule za mazoezi, shule ya msingi ya mazoezi na shule ya sekondari ya mazoezi, lakini zile shule zote sasa hivi zimerudi TAMISEMI. Sasa naomba kupata ufafanuzi kila kitu ambacho kilifanya muanzishe shule shule za mazoezi ambazo sisi tuliokuwa tunafundisha kule tuliona umuhimu wake kwa nini sasa hivi shule hizo zimerudishwa kupelekwa TAMISEMI?
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ule umuhimu umepotea ama kuna kuna kitu gani hapo kilichopo katikati? Tunaomba ufafanuzi kwa sababu mwenyewe nimesoma shule ya mazoezi ya msingi na katika miongoni mwa shule ambazo zilikuwa zinafanya vizuri ni shule za mazoezi na pia wale wanachuo wa ualimu walikuwa wanaenda kufanya practice kwenye shule za mazoezi. Lakini sasa hivi, ukitaka kuitumia ile shule ni lazima uende ukaombe kibali TAMISEMI na vitu kama hivyo, kwa hiyo kuna mzunguko mkubwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Bodi ya Mikopo. Mheshimiwa Waziri juzi nimekuona ukiitumbua TCU, mimi nasema umechelewa sana kwasababu malalamiko yalikuwa mengi ya muda mrefu. Watoto wa maskini ambao wana stahiki ya kupata mikopo hawapati, watu wanapeana mikopo kwa kujuana, tunaomba hilo suala ulifuatilie na wale wote waliohusika wawajibike na wale ambao walishindwa kusoma kwa sababu ya mikopo na sifa wanazo tunaomba wasome kwa sababu ni haki yao ya msingi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwenzangu asubuhi hapa ametoka kuongea, kuna vyuo vinafundisha masomo ya sayansi lakini havina maabara, Vyuo vya Ualimu. Tunategemea tunazalisha watu wa namna gani?
Mheshimiwa Mwenyekiti, huyo mwalimu leo unamfundisha kwa alternative to practical, unataka akifika shuleni umejenga maabara kwa kuwakimbiza wazazi, kwa michango mbalimbali, unataka akafundishe real practical, is it possible? If it is not possible we should be more serious ili elimu yetu tuione inapaa.
Mimi kila siku nasema masomo ya sayansi sio magumu ila mfumo wa elimu ya Tanzania ndio unapelekea masomo ya sayansi yawe magumu, masomo ya sayansi is very simple, ukipata mazingira wezeshi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ninaeongea hapa nimesoma PCB na nimefaulu kwani hao wanaofeli wamekosa kitu gani? Ni mfumo mbovu, mazingira mabovu, tunatakiwa tuone namna ya kuweka miundombinu yetu vizuri ili watoto wetu wasome kila mtu ana uwezo wa kusoma. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti …
Ahsante.