Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Spika, Mabadiliko ya Sheria milimita 10 mpaka milimita nane (8) nyavu za dagaa. Ni jambo jema kwa mabadiliko haya, lakini tatizo ni kubwa zaidi kwenye Ziwa Victoria kuliko bahari. Dagaa wanaopatikana katika Ziwa Victoria wana size ndogo kiasi kwamba, kuvuliwa kwa nyavu za milimita10 si sahihi na ni uonevu kwa wananchi wanaofanya kazi katika Ziwa Victoria. Ikumbukwe dagaa wanavuliwa kwa kuchotwa, kwa hiyo, mabadiliko haya yaguse pia, dagaa wanaovuliwa katika Ziwa Victoria ili pia, iruhusiwe kuvua dagaa kwa kutumia nyavu za milimita nane.

Mheshimiwa Spika, Samaki Wadogo Wasiokua zaidi ya Size iliyowekwa; naomba Kauli ya Serikali kuhusu uvuvi wa samaki kama furu, ngere na kadhalika. Samaki aina hii ni maalum sana kwa maeneo kama Ukerewe. Ikumbukwe kwamba, samaki hawa walianza kupungua baada ya kupandikizwa kwa sangara kwenye Ziwa Victoria, lakini badala yake wananchi ndio wanaadhibiwa kwa kuzuiliwa kuvua samaki hawa. Wananchi wa Ukerewe na maeneo mengine yanayozunguka Ziwa Victoria waruhusiwe kuvua samaki aina ya ngere, furu na wengineo ambao hawawezi kukua kufikia size inayowekwa na sheria.

Mheshimiwa Spika, Uvuvi wa Vizimba; urasimu ni mkubwa sana kwa watu wanaotaka kuwekeza kwenye vizimba na mchakato unagubikwa na rushwa. Kuna tozo nyingi sana mpaka kupata kibali, jambo linalokatisha tamaa. Hakuna uwekezaji wowote kwa watu hasa, vijana wanaoishi maeneo ya pembezoni mwa ziwa kama njia mbadala ya kuimarisha uchumi wa watu wetu.