Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Spika, awali ya yote namshukuru Mungu kwa zawadi ya uhai kwetu sote na utashi wa kujadili maendeleo. Nampongeza Mheshimiwa Waziri kwa juhudi nyingi za kuendeleza sekta hii, Naibu Waziri, Katibu Mkuu Mifugo, Katibu Mkuu Uvuvi na wakuu wote wa Idara na vyuo husika kwa kazi nzuri. Natoa shukrani kwa kampuni ya Asas, Iringa na Tanga Fresh, Tanga kwa ukarimu wa kutunywesha maziwa yao leo.

Mheshimiwa Spika, leo nitazungumzia ufugaji wa kuku wa kienyeji. Awali ya yote naomba ufafanuzi wa takwimu za mifugo ya nchi hii, iliyotolewa ukurasa wa nne aya ya 10. Hivi takwimu hizi zinapatikana vipi au ni za kwenye mashamba ya Serikali tu? Mimi ni mfugaji mdogo lakini sijawahi kutembelewa na afisa yeyote anayefanya sensa ya mifugo.

Mheshimiwa Spika, kwenye ukurasa wa sita mwanzo tunaelezwa kuwa kuku wa asili wameongezeka kutoka milioni 38.2 hadi milioni 38.5, hii ina maana kwa mwaka mzima ni kuku 300,000 tu wameongezeka. Tatizo ongezeko ni asilimia ndogo sana na ukizingatia kuwa kuku hawa wa asili ni rahisi sana kufuga kwani wao wana scavenge in their own na ni msaada kwa akinamama wa vijijini na vijana wetu wanaomaliza shule ambao hawana ajira. Mfano hai tumeona kwenye mradi wa TASAF. Swali, Serikali ina mpango gani kuwa na local chicken gene bank?

Mheshimiwa Spika, toka nimeingia Bunge hili la 11, kila mara namsumbua Waziri na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, jinsi ya kupata vifaranga hao wa kienyeji kwa ajili ya wanawake wa Kilimanjaro, lakini wananipa namba za simu ambazo hziajibiwi, ni lini sasa nitapatiwa vifaranga hao?

Mheshimiwa Spika, tatizo uchanjaji wa mifugo; ni takriban miaka 58 tangu tupate uhuru, lakini ugonjwa wa mdondo ukurasa wa sita, aya ya 16 inayosomeka mpaka ukurasa wa saba imeelezwa vizuri sana. Ni kwa nini Serikali haifanyi mass vaccination? Naona kwamba ni vyema chanjo hiyo na chanjo nyingine zote zikatolewa bure.

Mheshimiwa Spika, maeneo ya vipaumbele katika mpango na bajeti 2018/2019 ni pamoja na kudhibiti magonjwa ya mlipuko na magonjwa ya kipaumbele (page 13:iii) ni kwa nini isiwe kuondoa kabisa magonjwa hayo ili watu wa hali ya chini wafuge kuku wa kienyeji bila hofu?

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.