Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Jitu Vrajlal Soni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. JITU V. SONI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa fursa ya kuchangia siku ya leo. Awali ya yote nimshukuru Mwenyezi Mungu, lakini pia nimshukuru Rais wetu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa nia njema na jitihada kubwa anayofanya kuhakikisha kwamba jambo hili, Sekta ya Mifugo na Uvuvi iweze kuchangia katika pato la Taifa lakini pia kulinda maslahi ya wafugaji na wavuvi kwa ujumla. Pia niwashukuru na niwapongeze Waziri, Naibu Waziri na Katibu Wakuu wote kwa kazi kubwa na nzuri wanayofanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nishauri katika maeneo machache:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja; naomba tuendelee kujikita na kuboresha huduma mbalimbali kwa mfano ya veterinary, fedha iliyotengwa ni ndogo lakini tuangalie namna ya kuwapatia mikopo na nini ili huduma ya veterinary iendelee kufika katika maeneo mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ningeendelea kuomba Wizara hii ndiyo ina jukumu la kulinda ardhi zote za wafugaji, leo ardhi za wafugaji zinaendelea kuporwa na kubadilishwa matumizi na yanabadilishwa matumizi kutoka kwenye general land na kuingia kuwa maeneo ya hifadhi, lakini pia vijiji vinabadilisha matumizi ya ardhi ya wafugaji ambayo tayari yalishatengwa kabisa na yalipewa na hati, wanakaa kwenye mkutano kwa sababu wafugaji ni wachache, wanabadilisha hayo maeneo yanakuwa ni maeneo ya kilimo. Sasa ndiyo maana inaleta mgongano mkubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sehemu nyingine ambayo ningeomba nichangie ni blueprint. Ni vizuri Serikali ikasimamia kweye Sekta hii ya Mifugo na Uvuvi blueprint hasa tukiangalia kwenye suala la viwanda vya maziwa. Viwanda vya maziwa vinapata tatizo kubwa na vinashinda kushindana na maziwa kutoka nje kutokana na ada, tozo, kodi na ushuru mbalimbali. Jambo hili tusipoliangalia vizuri, viwanda hivi na hii ndoto yetu kubwa tutakuwa hatufikii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili tuwe na maziwa ya kutosha tushindane na wenzetu majirani, ningeomba kwenye kituo kile cha Nike tuwekeze fedha za kutosha, tuwapatie fedha ili waende kuhimilisha ng’ombe katika maeneo mbalimbali, tupate ng’ombe wazuri, bora na pia ule mpango wa kuzalisha mitamba 5,000 kwa mwaka, ningeomba Serikali iangalie kwa juhudi yoyote ile nje ya mfumo wa bajeti namna ya kuzalisha mitamba ya kutosha. Tukitaka kuwa na maziwa ya kutosha na ng’ombe wazuri, lazima tuwe na mifugo ya uhakika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini mbali na hiyo lazima Serikali wakae kwa pamoja kuangalia ule mnyororo wa thamani wa namna ya kuhifadhi bidhaa za uvuvi lakini pia mifugo, cold storage na chillers nayo waangalie namna ya kuboresha, kuwekeza humo na kuondoa kodi mbalimbali. Tatizo kubwa la wafugaji ni upatikanaji wa maji, majani ya uhakika (malisho), lakini hivyo hivyo njia pekee ya kufanya hivyo ni Serikali kuondoa kodi kwenye mitambo ya kuchimba maji, kutengeneza mabwawa na majosho. Hili siyo lazima Serikali ifanye, Sekta Binafsi wafugaji wakiwawekea mazingira wezeshi na niwapongeze kwamba wana leongo la kuunda ushirika wa wafugaji ili na wao wakakope kwenye Benki ya Kilimo, waweze kukopa kwenye Mfuko wa Pembejeo, wao wenyewe kutokana na mifugo tuliyokuwa nayo tutaweza kuwekeza. Tatizo kubwa linakuja Sekta isiyokuwa rasmi inaendelea kukua kutokana na hiyo blueprint, ada, kodi, tozo na ushuru mbalimbali. Hatutafanikiwa kama wasipokaa na kuangalia namna ya kuboresha jambo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia niwapongeze kwenye suala la aqua culture, wanafanya vizuri. Ningeomba elimu hiyo iendelee kutolewa na watusaidie katika maeneo mbalimbali ili tukuze pato la Watanzania kwa wingi, lakini pia wapate chakula na bidhaa za kufanyia kazi kwenye viwanda vyetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hapo, naunga mkono hoja, mengi nitaandika kwa maandishi. Ahsante sana. (Makofi)