Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

Hon. Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Spika, Mradi wa Umwagiliaji wa Suga uliopo katika Kata ya Suga Wilayani Ulanga umejengwa miaka mingi lakini umeshashindwa kufanya kazi hivyo kuitia Serikali hasara.

Mheshimiwa Spika, Kuhusu Mradi wa Minepa. Mradi huu upo Kata ya Minepa na umeshaanza kazi, lakini gharama za mradi na ubora wake haviendani kabisa na kuna malalamiko mengi kutoka kwa mkandarasi.

Mheshimiwa Spika, Kuhusu Mradi Mkubwa wa Lupiro. Huu ndio mradi utakaolikomboa eneo la Wilaya ya Malinyi, Ulanga na Kilombero. Tayari tafiti zilishafanyika na thamani ya mradi ni bilioni 52, hivyo tunaomba fedha.