Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, Mradi wa Scheme ya Umwagiliaji ya Mtula. Baada ya umwagiliaji kuhamishiwa Wizara ya Kilimo, ninaomba Serikali ione uwezekano wa kukamilisha Scheme ya Umwagiliaji ya Kijiji cha Mtula ambayo ni msaada mkubwa kwa kilimo na uchumi wa wananchi wa Mafinga.

Mheshimiwa Spika, uchumi wa viwanda, msingi wake ni kilimo; jitihada za kujikwamua na uhaba wa sukari, zitafanikiwa ikiwa tu Wizara ya Kilimo itaongeza jitihada za kilimo cha miwa hasa kwa small scale na hasa kwa kufanya ubia kati ya Serikali (halmashauri na sekta binafsi).

Mheshimiwa Spika, naambatisha haya maelezo ya Kaimu Mwenyekiti wa Chama cha Wakulima wa Miwa, Dkt. George Mlingwa, na wenzake. Pamoja na kuwa andiko hili ni la mwaka 2016/2017 bado ninaamini module hii ambayo wenzetu Brazil wametumia inaweza kuwa suluhisho la uhaba wa sukari ambao msingi wake ni kilimo cha uhakika cha miwa.

Mheshimiwa Spika, maelezo kwa ufupi kuhusu sukari, kuna maeneo mengi nchini ambayo tunaweza kujenga viwanda vidogo na vya kati, (tani 10,000 mpaka tani 30,000 kwa mwaka). Kila mkoa una maeneo kama haya. Kwa mfano Kilosa tani 10,000, Manyara tani 10,000, Mara tani 30,000, Ruvuma tani 10,000, Dodoma Chamwino tani 10,000, Kigoma Bonde la Malagarasi tani 30,000, Pwani – Rufiji tani 30,000 na kadhalika.

Mheshimiwa Spika, uendelezaji wa viwanda vidogo unachukua muda mfupi, miezi nane mpaka kumi. Gharama zake ni za chini USD milioni tatu hadi kumi ukilinganisha na vile vikubwa USD milioni 100 hadi milioni 300 ambavyo huchukua miaka miwili hadi mitano. Viwanda vidogo viko karibu na wananchi, bei ya sukari yake ni nafuu kutokana na gharama kuwa chini. halmashauri za wilaya husika zinaweza kuingia ubia na wawekezaji wazalendo katika maeneo yao. Miradi hii inaweza kuziingizia mapato halmashauri zetu.