Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

Hon. Jitu Vrajlal Soni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

MHE. JITU V. SONI: Mheshimiwa Spika, awali ya yote naomba nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa siku ya leo kupata fursa ya kuchagia na kunipa afya njema.

Mheshimiwa Spika, nichukue fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu pia kutupa Baraka zake nchini na kutupa amani.

Mheshimiwa Spika, nimpongeze Rais wetu wa Awamu ya Tano Mheshimiwa John Pombe Joseph Magufuli pamoja na Mawaziri wake hasa katika Wizara ya Kilimo, Katibu Mkuu, Wakurugenzi wa taasisi mbalimbali chini ya Wizara hii muhimu.

Mheshimiwa Spika, napenda kushauri katika maeneo mbalimbali ili kuboresha sekta ya kilimo.

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nashauri suala la bajeti, kwa maoni yangu kila mwaka bajeti ya Wizara hii hushuka kidogo kidogo. Maelezo tunayopewa ni kupanda kwa bajeti ya Wizara nyingine zinazopeleka pia bajeti zao kwa maendeleo ya wakulima. Mimi binafsi nikipiga hesabu kutokana na Bajeti kuu ya Shs. trillion 33, hiyo mikataba tuliyoingia kama nchi, ya Malabo na Maputo kufanya asilimia 10 ya bajeti tatu kwa sekta ya kilimo, bado hatujafikia asilimia 10 ya trillion 33, ni trillion 3.3. Hata ukijumlisha fedha zote za Wizara mtambuka kama TAMISEMI, Ardhi, Mifugo na Uvuvi, (Barabara za vijiji) uchukuzi, Maliasili na Utalii, Maji, Mawasiliano, Elimu, Afya, Fedha zinazokwenda vijijini tulipo wakulima haziendi trillion 3.3 (chukua, Bajeti za REA, TARURA, RUWASA, Afya, Elimu, TAMISEMI)

Mheshimiwa Spika, pia ukilinganisha Bajeti za Kilimo kwa miaka mitatu au mitano, badilisha kwa bei hiyo ya Dollar ya Marekani ($USD) utanona bajeti inashuka.

Mheshimiwa Spika, pili nashauri Serikali itekeleze “Blueprint” ili kuondoa tatizo la urahisi wa kufanya biashara (Fair Competition in Trade). Leo hii tumeona sekta isiyokuwa rasmi inakua kutokana na sekta rasmi kutozwa kodi, Ada, Tozo na ushuru mkubwa na kwa idadi kubwa kutoka kila taasisi ya udhibiti (Regulatory Bodies).

Mheshimiwa Spika, nashauri Serikali iangalie namna ya kuboresha sekta ya umwagiliaji. Nipongeze Serikali kurudisha sekta ya umwgiliaji. Niipongeze Serikali kurudisha Tume ya Umwagiliaji kutoka Wizara ya maji kurudi Wizara ya Kilimo. Naamini Wizara hii itaitendelea haki sekta ya umwagiliaji tangu Tume kuanzishwa hadi leo haikupangiwa au kupewa fedha za maendeleo katika umwagiliaji. Nashauri Serikali isibaki kujaribu kufanya peke yake bali iweke mazingira wezeshi na rafiki ili sekta binafsi pia ichangie. Nashauri Serikali iondoe kodi katika mitambo ya kuchimba maji na mitambo ya kutengenezea mabwawa, pamoja na kodi ya Pump za Sola za umwagiliaji na vipuri vya zana za umwagiliaji. Pia Benki ya TADB na Mfuko wa Pembejeo watenge asilimia 20.

Mheshimiwa Spika, nashauri kila Mkoa upewe angalau mitambo ya kuchimba mfereji na mabwawa badala ya kutoa tenda ya kuchimba maji na kutengeneza mabwawa.

Mheshimiwa Spika, napongeza juhudi ya kuwa na Sera na Sheria ya Kilimo, ndiyo njia pekee ya kusonga mbele. Hapa nashauri ardhi ya kilimo italindwa na mijini mashamba ya kilimo yataendelea.

Mheshimiwa Spika, nashauri TARI ipewe kipaumbele kwa kupewa bajeti ya kutosha ya ndani ili wenye kufanya utafiti vizuri wa mbegu, viuatilifu vizuri vya mbegu, viuatilifu vya magonjwa na pia ugani katika kilimo. Bila kuwekeza katika taaisi yetu ya TARI kilimo chetu itabidi kuwa cha kubabaisha na duni bila tija. Tuna vituo 17 na vyote vinahitaji kuboresha miundombinu, vifaa vya kisasa kufanya kazi zao vizuri na zana nyingine kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi. Nashauri Chuo Kikuu cha SUA kiwe chini ya Wizara ya Kilimo ili kuboresha tija katika chuo hicho.

Mheshimiwa Spika, nashauri ASA iongezewe mtaji ili kuzalisha mbegu bora na zenye viwango kwa kutosheleza mahitaji ya nchi. Nje ya bajeti wao wakopeshwe zana za Kilimo, matrekta na zana nyingine, vifaa vya umwagiliaji vya aina mbalimbali kutokana na shamba husika, vifaa vya kuchakata na kusafisha mbegu na kuweka dawa ya kuhifadhi na kutunza mbegu na hapo hapo TASTA pia ipewe watumishi wa kutosha na wapate mfumo wa TEHAMA kwa ajili ya kusafirisha mbegu za ndani na nje ili kuwa na udhibiti wa uhakika.

Mheshimiwa Spika, pia na shauri TFS wafanye uhakiki wa aina mbalimbali za mbolea na kuishauri Serikali kuondoa vikwazo katika baadhi ya vipengele kwenye Sheria ya Mbolea.

Msheshimiwa Spika, nashauri Serikali na Wizara ishirikiane na taasisi nyingine kuboresha TPRI iliyopo chini ya Wizara ya Kilimo na kuiboresha pia Miundombinu, vifaa vya kisasa kuifanya kazi yao. Wafanye utafiti wa mabaki ya sumu tunayotumia sisi walaji wa mazao (Nop pesticide Residuals) na kushauri nini kifanyike.

Mheshimiwa Spika, mwisho, Benki ya Kilimo na Mfuko wa Pembejeo ziongezewe mtaji ili Serikali ifanye yale yake na sekta binafsi zifanye juhudi kuendeleza kilimo na umwagiliaji.