Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

Hon. Sonia Jumaa Magogo

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

MHE. SONIA J. MAGOGO: Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kwa kuipongeza Wizara kwa jitihada kubwa wanazofanya katika kukuza kilimo nchini.

Mheshimiwa Spika, nianze kwa changamoto ya ahadi wanazopewa wakulima lakini zinageuka kuwa vilio. Mfano ni Mkoa wa Tanga; mwaka 2018 walipewa ahadi wakalima mihogo kwa kiwango kikubwa sana mwisho wake ikageuka hasara kubwa kwao. Hamasa hii ilitoka kwa baadhi ya viongozi wa Serikali na mashirika yasiyokua ya kiserikali. Tatizo hili liliwapata pa wananchi wa Tunduma kwenye kilimo cha mbaazi. Niiombe Serikali iliangalie hili tatizo na kuona inazuiaje lisijirudie, na pia kuwasaidia wale wanaokumbwa na hasara hii kwa kuwafidia walau kwa kiwango fulani ili wasikate tama maana kilimo ndio uti wa mgongo kwa nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, pia niiombe Serikali ione umuhimu wa kuwaelimisha na kuwapa hamasa hasa vijana ambao ndio wana nguvu kujiunga sana na kilimo kwa kuwasaidia pembejeo, elimu na maeneo ili kuwavutia wasizagae tu mitaani kwa kukosa ajira rasmi hatimaye kujiajiri katika kilimo.

Mheshimiwa Spika, vilevile wakulima wa mbogamboga wengi wao wanalima katika mabonde ya maji machafu, labda ni kwa kukosa elimu ya afya au kukosa maeneo hivyo kupelekea matatizo ya kiafya kwa watumiaji wa mboga hizo ikiwemo kuumwa matumbo.

Mheshimiwa Spika, wananchi wengi wanalima tu kimazoea bila kuwa na elimu ya kilimo bora. Serikali ione umuhimu wakuwaelimisha wakulima kwa ngazi za vijiji maana si wote wana uwezo wa kusikiliza kupitia redio au televisheni.

Mheshimiwa Spika, lakini kabla ya kumalizia niiombe Serikali iwasaidie sana wakulima pembejeo za kilimo kwa wakati. Naomba kuwasilisha.