Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

Hon. Anthony Calist Komu

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

MHE. ANTONY C. KOMU: Mheshimiwa Spika, kwanza nipongeze uongozi mzima wa Wizara kwa jitihada wanazofanya kukabiliana na changamoto mbalimbali katika sekta ya kilimo pamoja na ufinyu wa raslimali walizonazo.

Mheshimiwa Spika, ili tuweze kufanya mapinduzi ya kilimo katika Taifa letu ni lazima tuamue kama Taifa kwa makundi kuwekeza vya kutosha katika kilimo na hususani katika Nyanja ya umwagiliaji.

Mheshimiwa Spika, katika Jimbo langu la Moshi Vijijini kwa miaka mingi tulishaingia katika kilimo cha umwagiliaji na kwa bahati nzuri tulipata mradi mkubwa wa umwagiliaji kwa ushirikiano na nchi ya Japan Mradi unaoitwa Moshi Irrigation Scheme. Mradi huu umekuwa ni mkombozi mkubwa kwa watu wetu hasa katika Kata za Mabogini, Arusha chini na Old Moshi Magharibi.

Mheshimiwa Spika, mradi huu sasa unakabiliwa na changamoto kuu tatu.

(i) Maji hayatoshi hivyo zinahitajika fedha kwa ajili ya kuboresha miundombinu iliyopo katika mradi huu kuepusha maji mengi kupotea na kulinda vyanzo vya maji hayo.

(ii) Wakulima wa mpunga katika mradi huu wameunda ushirika wao na kwa muda mrefu wamekuwa wakiomba wakabidhiwe vifaa vilivyoachwa wakati wa kuanzishwa kwa mradi huu ikiwa ni pamoja na mashine ya kukoboa mpunga mpaka leo hawajakabidhiwa mashine.

Mheshimiwa Spika, naomba Waziri afanye kila linalowezekana wakulima hawa wajibiwe kilio chao.

Mheshimiwa Spika, changamoto ya tatu ni barabra inayoingia katika mradi huu inayoitwa Funga Gate – Mabogini – Chekereni – Kahe; kipindi kirefu cha mwaka barabara hii haipitiki kabisa jambo ambalo linaathiri sana ustawi wa mradi huu.

Mheshimiwa Spika, katika mpango wa kuendeleza kilimo awamu ya pili zipo fedha zilizoainishwa kwa ajili ya kuboresha miundombinu katika miradi ya umwagiliaji. Naiomba Wizara iratibu vizuri fedha hizi na kwa kushirikiana na TARURA ili barabara hii iweze kutengenezwa ikiwezekana kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa mifereji ya asili huko nyuma imekuwa ikisaidiwa katika ukarabati wake na Serikali kupitia Ofisi ya Kanda ya Tume ya Umwagiliaji. Kwa muda mrefu support hii imekoma matokeo yake ni kwamba mifereji mingi imeanza kufa jambo ambalo ni hatari sana kwa ustawi wa watu wa Moshi Vijijini. Mifereji kama Makeresho wa Kata ya Kibosho Magharibi, mfereji wa Makupa, Metro na mingine mingi karib kata zote 16 inahitaji ukarabati mkubwa.

Mheshimiwa Spika, naiomba sana Wizara irejee utaratibu wake wa zamani wa kusaidia mifereji hii kwa kuwa mahitaji ya sasa wananchi hawawezi kuyamudu kwa nguvu zao wenyewe.