Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

Hon. Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Spika, Utafiti wa mbegu mpya na TARI–GMO ya Malindi katika Kituo cha Makutupora Dodoma. Napongeza hatua hiyo lakini kumekuwa na kauli kinzana Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo alinukuliwa akisema Serikali imepiga marufuku majaribio ya GMO, huku hotuba ya Waziri ikionesha kuwapongeza Wizara imegundua mbegu mpya za mahindi inayostahimili magonjwa.

Mheshimiwa Spika, Bajeti ya Wizara ya maendeleo inayoombwa na Wizara ya kiasi inayopelekwa ni asilimia 48.74. Hata nusu ya asilimia hamsini haifiki kama nchi, kilimo sio kipaumbele na hii inajidhihirisha kutokana na bajeti ndogo iliyopelekwa na hata hii inakiuka makubaliano ya Malabo kuna bajeti ya kilimo lazima itengwe na kufikiwa kwa asilimia 10 ya bajeti.

Mheshimiwa Spika, ASA; Serikali iongeze nguvu kusaidia utafiti wa mbegu katika vituo vya utafiti. Sasa hivi mbegu nyingi zilizopo nchini hazitoshelezi badala yake makampuni binafsi kama SEDICO, Panner na kadhalika ndio makampuni yanayosambaza mbegu nchini. Ikumbukwe kuwa Harb za makampuni haya ya nje zipo nje ya nchi hivyo ikitokea siku wakagoma ku-supply mbegu nchini hatutakuwa na sustainable agriculture, lazima Serikali ifikirie.

Mheshimiwa Spika, kuwekeza kwenye uzalishaji wa mbegu mfano Kenya ilivyofanya kwamba Agricultural Institute zinatengewa bajeti ya kutosha na kuwekeza nguvu kwenye utafiti wa mbegu za kilimo, mbogamboga matunda.

Mheshimiwa Spika, kodi nyingi kwenye kilimo, mfano kilimo cha tumbaku zimezidi mfano (Cess/city service, skills development levy, tozo ya Bodi za Kusindika, tozo Bodi ya Kununua Zao Mbichi, export levy, radiation levy, ushuru wa ushirika, ushuru wa research, halafu mkulima alipwe malipo ya pili all on top of the price, nchi nyingine mkulima analipwa bei anahangaika na kodi kwani yeye sio mnunuzi.

Mheshimiwa Spika, Viwanda vya Tumbaku Morogoro vinapunguza ununuzi wa tumbaku kutokana na Serikali kushindwa kulipa 25 bilioni returns VAT; iko haja Wizara ya Kilimo na Viwanda na Biashara kufanya kazi kwa pamoja maana viwanda vikifa wakulima hawatakuwa na wanunuzi wa mazao yao.

Mheshimiwa Spika, upotevu wa mavuno (post harvesting) wakulima wengi wanapoteza mazao yao kutokana na ukosefu wa maghala ya kuhifadhi mazao. Hali hii ya kukosekana maghala kunasababisha wakulima kulazimika kuuza mazao yao kwa bei ya kutupwa/bei ya hasara. Ushauri, Serikali ifikirie kujenga maghala makubwa katika maeneo ambayo yana kiwango kikubwa cha mazao.

Mheshimiwa Spika, mikopo ya matrekta kwa wakulima; bila kufanya utafiti wa kutosha wakulima wengi wanashindwa kurejesha mikopo. Mfano wakulima waliopo milimani wamekopeshwa matrekta hawawezi kuyatumia hali inayosababisha wakulima kupaki matrekta juu ya mawe, mfano wakulima wa Mgeta, Mvomero Mkoani Morogoro ni vyema utafiti wa kina wa matumizi ya matrekta hayo ukafanyika kabla ya kutoa mikopo hiyo.