Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

Hon. Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

3

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, mkonge; pamoja na mchango wangu wa kuzungumza naomba nishauri Serikali kwa Wizara ya Kilimo na Fedha kukaa pamoja ili kuweka kwenye Finance Bill kipengele cha namna ya kutoza produce cess kwa wakulima wote wakubwa wanaosafirisha nje mkonge ili tusiwavunje moyo wanunuzi wanaokuja kununua mkonge wa wakulima wadogo. Pia fedha hizi zitasaidia utatuzi wa changamoto za zao la mkonge.

Mheshimiwa Spika, chai; kumekuwa na changamoto ya upatikanaji wa pembejeo kwenye zao la chai. Jambo linalowalazimisha wakulima kukopa pembejeo kwa wenye viwanda na kuwaathiri kwenye bei. Ushirika katika chai uimarishwe , pia tuanzishe soko au mnada wa chai hapa nchini.

Mheshimiwa Spika, umwagiliaji; ili kuwaondoa katika umaskini wananchi wa kata 10 za Tarafa ya Mombo ni kutekeleza Mradi wa Umwagiliaji wa Bonde la Mto Mkomazi. Bwawa linaloweza kusaidia kilimo cha umwagiliaji kwenye hekta zaidi ya 5,000.

Mheshimiwa Spika, Bodi ya Mkonge, kumekuwa na udhaifu mkubwa wa usimamizi wa mkonge kwa sababu ya uwezo mdogo wa Bodi ya Mkonge. Nashauri bodi iangaliwe upya. Pia Serikali ifuatilie utaratibu uliotumika kutoa mashamba ya mkonge. Pia namna mali za Bodi ya Mkonge zilivyouzwa au kugawanywa ili kujua Bodi ilikuwa na mali gani, zimekwenda wapi na kwa utaratibu upi?