Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

Hon. Dr. Haji Hussein Mponda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

MHE. DKT. HAJI H. MPONDA: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja na naipongeza Wizara kwa ujumla katika utekelezaji wa majukumu ya Wizara pamoja na changamoto ya ufinyu wa bajeti.

Mheshimiwa Spika, Serikali imejenga skimu ya umwagiliaji ya Itete katika Wilaya ya Malinyi (2011-2013). Toka skimu hiyo kukamilika na kukabidhiwa kwa wananchi katika Vijiji vya Minazini, Alabama na Itete, skimu hiyo haitumiki kwa kikamilifu kutokana na changamoto za upungufu wa maji, mitaro mibovu na ukosefu wa barabara kuelekea katika mashamba ya skimu hiyo.

Mheshimiwa Spika, Serikali mwaka 2015 na 2016 ilikiri kabisa kwamba skimu hiyo imejengwa chini ya kiwango stahiki na kuahidi kuifanyia marekebisho upya ili skimu itumike kikamilifu. Naiomba Serikali itekeleze ahadi ya ukarabati au marekebisho ya skimu hiyo katika bajeti ya mwaka huu 2019/ 2020 kama ilivyoahidi.

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Malinyi bado ina fursa kubwa ya ujenzi wa skimu zingine katika Mito ya Lwasesa, Sofi, Furua, Mwatisi na mingineyo. Je, ni lini Serikali itafanya utaratibu wa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina katika mito hiyo minne ili ititirishe maji ya uhakika masika na kiangazi ili ujenzi wa skimu za umwagiliaji uanze. Ahsante.