Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

Hon. Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Spika, nachangia mambo yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza, umuhimu wa uwekezaji katika utafiti; ni muhimu sana kuwekeza katika utafiti hasa kubaini aina ya udongo na kutambua/kushauri ni aina gani ya mazao yalimwe na kupandwa kwenye eneo husika. Jambo hili litasaidia kufanya kilimo chenye tija na mazao mengi yatakayotokana na ushauri wa kitaalam. Mfano, Visiwa vya Ukerewe vyenye eneo la kilomita za mraba 6400, ni asilimia 10 tu ambayo ni nchi kavu. Kwa sababu ya kilimo cha kujirudiarudia hatimaye sasa ardhi yake imechoka na haina rutuba tena. Zao kuu ambalo ni muhogo halistawi tena pamoja na mazao mengine.

Mheshimiwa Spika, hivyo, Wizara pamoja na maeneo mengine inatakiwa ipeleke wataalam wake visiwani Ukerewe ili wafanye utafiti wa kisayansi kubaini aina ya udongo na kushauri yapandwe na kwa utaratibu upi. Jambo hili itasaidia eneo letu dogo litumike kwa ufanisi na kwa tija na kuondoa tatizo la upungufu wa chakula kwenye Visiwa vya Ukerewe.

Mheshimiwa Spika, uwekezaji na umuhimu wa umwagiliaji, ni jambo lililo wazi kwa kuwa zama za kufanya kilimo cha kutegemea mvua kimepitwa na wakati. Kwa kuwa nchi yetu imebahatika kuwa na vyanzo vingi vya maji ni vizuri sana kuwekeza zaidi kwenye kilimo cha umwagiliaji tukitumia vyanzo hivi vya maji. Mfano, Visiwa vya Ukerewe ambavyo vimezungukwa na maji havitakiwi kuwa na shida ya chakula na vingeweza kuhudumia maeneo mengine kwa chakula kama tu Wizara ingewekeza kwenye umwagiliaji. Mradi wa umwagiliaji wa Miyogwezi na Bonde la Bugorola umesimama kwa sababu ya kukosa fedha.

Mheshimiwa Spika, ushauri, Wizara ifufue mradi wa umwangiliaji Miyogwezi na Bungorola ili kutumia rasilimali maji yaliyopo Ukerewe na kuifanya Ukerewe kuwa wazalishaji wakubwa itakayofanya wajitoshereze kwa chakula na ikiwezekana kuhudumia maeneo mengine kwa chakula.