Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

Hon. Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Spika, mchango wa Sekta ya Kilimo ni mkubwa na muhimu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, 30% ya Pato la Taifa; 30% ya bidhaa zinazouzwa nje; 65% ya malighafi za viwanda; 65.5% ya ajira; na 100% ya chakula kudhibiti mfumuko wa bei. Hivyo kilimo ni muhimu katika kuifikisha Tanzania yetu kwenye Dira ya Tanzania ya 2025 kuwa na uchumi wa kati, Tanzania ya viwanda.

Mheshimiwa Spika, ikiwa hivyo ndivyo ilivyo, inabidi kuimarisha kilimo na upatikanaji wa chakula uwe na uhakika. Namna ya kuimarisha kilimo kwa kufanya utafiti wa kweli wa udongo, mazao na teknolojia sahihi ili kuwa na masoko ya uhakika na kuwa na bei ambayo inafanya wakulima wapate faida ya kukuza kilimo.

Mheshimiwa Spika, sasa hivi kilimo kinakuwa kwa 3.1%; Malaba ilitaka kilimo kikue kwa 6% na uwekezaji wenye kilimo ufikie 10% ya Pato la Taifa. Sasa uwekezaji kwenye kilimo ni chini ya 5%, Serikali isaidie. Tatu, wakulima wanahitaji Wagani kwa kila kijiji watosheleze mahitaji yao. Sasa hivi kuna vijiji vingine havina Wagani, naomba Serikali Wagani wote waliofuzu waajiriwe kuongeza nguvu ya wakulima ya kuzalisha mazao.

Mheshimiwa Spika, nne, kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna. Sasa upotevu wa mazao unafikia kati ya 30% - 40%. Hii inawaletea wakulima hasara na hata Taifa. Najua Serikali inajitahidi kupunguza upotevu lakini bado jitihada inatakiwa zaidi.

Mheshimiwa Spika, tano, suala muhimu ni kuimarisha na kuongeza miundombinu ya umwagiliaji kutokana na mabadiliko ya tabianchi. Hanang iliomba kujengewa bwawa la Gidahababieg. Tumeomba bwawa hili ili kusaidia eneo la Gidahababieg kupata fursa ya kulima kwani ni eneo lenye uhaba wa mvua. Vilevile, bwawa hili linajengwa katika eneo ambalo maji yote ya mvua kutoka Mlima Hanang yangekusanywa. Huu ni mwaka wa kumi toka watu wa Hanang kupitia kwa Mbunge wameomba kujengewa bwawa. Nataka kujua kwa nini tumecheleweshewa bila kupata maelezo ya kuchelewesha ujenzi wa bwawa hili, itabidi nitoe shilingi.