Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

Hon. Suzana Chogisasi Mgonukulima

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

MHE. SUZANA C. MGONUKULIMA: Mheshimiwa Spika, kuhusu mawakala wa pembejeo kwa msimu wa mwaka 2015/2016; Serikali haijawalipa fedha wasambazaji pembejeo na kila mwaka Wizara ya Kilimo inapitishiwa bajeti, ndani ya miaka minne bado Serikali imeendelea kuhakiki, kama siyo uonevu kwa mawakala hawa. Niombe wakati Waziri anakuja kuhitimisha nipate kauli ya Serikali kwa bajeti ya mwaka 2019/ 2020 italipa madai hayo.

Mheshimiwa Spika, kuchelewa kwa upatikanaji wa mbolea kwa wakati na isiyo bora; ni kwa muda mrefu sasa ndani ya nchi yetu mbolea inachelewa kupatikana kwa wakati ili mazao yaweze kupatikana. Azma ya Tanzania kuwa nchi ya viwanda haiwezi kutimilika kama kilimo kitafanyiwa mzaha.

Mheshimiwa Spika, asilimia 75 ya Watanzania ni wakulima, wanatakiwa wapate mazao ya kutosha ili waweze kusomesha, kujitibu na kadhalika, lakini wakulima hawa wanalima bila msaada wa Maafisa Ugani, Serikali haioni kuwa imewaacha wananchi walime kilimo cha mazoea kisicho na tija, kwa kufanya hivyo hatuwezi kushindana na nchi za Umoja wa Afrika Mashariki, ina maana Tanzania tutabaki nyuma.