Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

Hon. Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Spika, pamoja na kutambua kuwa kilimo ni uti wa mgongo kwa nchi yetu, kwa nini wananchi zaidi ya asilimia 70 ni wakulima. Ambao wengi wao ni waelewa wa uwezo wa kati wa kuwa na maeneo makubwa na uzalishaji kuwa wa wastani, ni dhahiri wanahitaji kupewa elimu na kufanyiwa utafiti wa udongo kwa mazao yao, kutokukana na uchovu wa udongo wao. Hivyo Taasisi yetu ya TARI inahitajika kupatiwa fedha za kutosha kwani, hivi sasa tunahitaji utaalam wao zaidi ndani ya nchi yetu, hasa Mkoa wa Rukwa kwani mwaka 2018/2019 baadhi ya wakulima wamepatiwa mbegu zisizo bora na pembejeo kuwa feki na kumpatia hasara kubwa mkulima wetu.

Mheshimiwa Spika, nasikitika ndani ya ukurasa 20-23, TARI wameandaa nyenzo tatu za kumsaidia mkulima kufanya uamuzi wa kuboresha uzalishaji wa zao la mhogo, hakuna maeneo ya Mkoa wa Rukwa katika kufanikiwa na utafiti huo wa TARI kwa wakulima wetu wa mhogo - mwambao wa Ziwa Tanganyika, Kala, Wampembe, Kisumba-Kasanga, Karogwe, Kabwe, Kirando, Kipili, Mpombwe na kadhalika. Tunahitaji msaada wa zao hilo, kwani hatuna Maafisa Ugani wa kutosheleza mahitaji.

Mheshimiwa Spika, upungufu wa Watafiti na Maafisa Ugani tulishughulikie katika ajira yao ili tuboreshe kilimo chetu. Vijiji zaidi ya elfu 15, Maafisa Ugani ni elfu saba ni kujidanganya wenyewe.

Mheshimiwa Spika, ndani ya ukurasa wa 25, kuhusu mazao ya jamii ya mikunde, inalimwa kila pande ya nchi yetu na wananchi hutumia kama mboga kwenye chakula kikuu kwa kila upande. Uzalishaji wake unashuka pamoja na kutumika eneo kubwa la kuzalishia ni ukosefu wa mbegu bora. Bado uwezo ni mdogo wa TARI kuzalisha mbegu bora, si sahihi kwa wakulima 10,160,577 tu ndiyo wanufaika wa mbegu bora za aina ya mikunde. Ni vema nguvu ya rasilimali fedha kuandaliwa upya kwa maslahi ya wakulima wa nchi hii. Kuinua tija kwa wakulima wetu, hatuwezi kuwa tegemezi wa ukulima wetu.

Mheshimiwa Spika, tunaomba uwepo utaratibu maalum wa ujenzi wa maghala makubwa na vihenge vikubwa vya kutosha kwenye maeneo ya uzalishaji mkubwa. Majengo hayo ya Serikali yanapohifadhiwa mazao hayo hakuna uharibifu mkubwa, kuliko tunavyohifadhi wakulima wenyewe mazao uharibika na kupata hasara.

Mheshimiwa Spika, utafiti na ukaguzi wa karibu zaidi wa pembejeo za kuhifadhi mazao, nyingi ni fake. Asilimia 14.5 ya utekelezaji wa vihenge nchini, ni wa hali ndogo sana ambayo inakatisha tamaa kwa wakulima wanapoharibikiwa mazao yao. Tuongeze nguvu na usimamizi wa karibu. Pia Mkoa wa Rukwa tufikirie kuletewa hivyo vihenge vya kututosha. Tunasisitiza tujipange hasa na ujenzi wa maghala makubwa, kwa ajili ya stakabadhi ghalani ni zoezi limpatialo mkulima faida kwa mazao yao.

Mheshimiwa Spika, naomba kuunga mkono hoja.