Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

Hon. Katani Ahmadi Katani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tandahimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

MHE. KATANI A. KATANI: Mheshimiwa Spika, nichukue fursa hii kwanza kukushukuru, lakini nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kupata fursa ya kuchangia kwenye Wizara hii ya Kilimo. Moja niipongeze Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko ambayo iko Mtwara kwa kiasi kikubwa kwa fedha ndogo ambazo wamepewa wameweza kusimamia vizuri na kuwafikia watu japo tatizo la fedha ya korosho kwa wakulima limekuwa kubwa. Na hili nadhani linafahamika vizuri nilizungumza wakati nachangia Wizara ya Viwanda lakini leo narudia tena kwa Wizara yenyewe ya Kilimo. Leo tunapozungumza simu yangu hapa nikikuletea ina message zaidi ya 700 watu wanalalamika hawajapata fedha, tatizo limekuwa ni fedha. Sasa Wizara ya Kilimo mtusaidie mkishirikiana na wenzenu wa Biashara tatizo la fedha ya korosho kwa wakulima lini zitapatikana fedha zikawafikia wakulima wakaweza kupalilia mikorosho. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niliwaambia leo mikorosho watu wanakodisha shamba la heka 100, heka 80 mtu anakodisha kwa milioni tatu ili mradi tu aone kwamba sasa sina cha kufanya, watu wameshindwa kuwapeleka watoto shule kwa ajili ya fedha ya korosho hakuna, watu wameshindwa kufanya parizi la mikorosho kwa sababu ya fedha hakuna, lakini kuna shida ambayo naiona, nilisema ukienda maeneo ya Lindi kwa Mheshimiwa Nape, ukienda Kata ya Nachunyu leo korosho zinahitaji kupulizwa watu wale hawana dawa kwa sababu hawana fedha sijui Serikali inataka kutueleza nini wakati mna- wind up mtuambie mkakati thabiti wa fedha za wakulima wa korosho zitakwenda lini. Tunajua kazi mnaifanya kubwa kwa sababu jambo lenyewe hamkujiandaa nalo, kazi mnayoifanya kubwa lakini tatizo la fedha ni kubwa kuliko linavyodhaniwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, na hata maelezo na takwimu niliwahi kukwambia Mheshimiwa Waziri kwamba takwimu mnazozitoa mara nyingi haziko sahihi, ukienda Tandahimba rejection ya Benki imekuwa kubwa. Kwa hiyo, kitakachozungumzwa kimelipwa ukienda kwenye uhalisia ni tofauti kabisa Watanzania hawa wakulima wa korosho dhamana yao na azma yao ya kupata fedha ni lini? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nikubaliane na mawazo yenu mliyosema kwamba tuweke bima. Bima inaweza ikasaidia kwenye mazingira kama haya tunayokuwa nayo, ingetusaidia sana lakini bahati mbaya sisi Wabunge tuna bima za kila aina lakini kwa wakulima wa korosho ambao ndio nguvu kazi ya nchi hii hawana bima. Linapotokea anguko la biashara ya korosho kama hili hatuna kwa kukimbilia sasa niwaombe sana muone utaratibu na namna nzuri ambao mnaweza mkaweka jambo hili sawa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilizungumza Wizara ya Biashara suala la Kangomba na nyie ndio wenye korosho wenyewe nataka niwaambie kwenye korosho kule wakati wa korosho kuna wakinamama wanauza mchele wanabadilisha kwa korosho yaani ni butter trade system ipo, Mheshimiwa Mgumba umekaa kwenye korosho unayajua haya mnapokaa mkazungumza mambo ya kangomba na nyie watu wa kilimo mpo na mpo mliokaa kwenye korosho Mheshimiwa Omary umekaa kwenye korosho unajua, wakinamama wanapika maandazi wanabadilishana korosho.

Mheshimiwa Spika, kesho akipeleka korosho unatka kuonesha shamba ni kweli haya mambo mnayoyafanya? Haya kweli mnayoyafanya yako sahihi? Butter trade system ipo kwenye Mpunga, ipo kwenye Kahawa, ipo kila mahali ambapo mkulima anafanya biashara, sitarajiii itatokea miujiza tena ya kukaa mtu ukazungumza Kangomba japo Mheshimiwa Waziri unasema utatafutwa mfumo rasmi wa kurasimisha kangomba iwe jambo ambalo lipo kisheria. Lakini kwenye biashara hii hakuna jambo hilo haliwezekani yaani haupo utaratibu ambao utaupata ukasema hili unataka uliweke kisheria kwa sababu sheria hiyo itakataa tu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo ulivyosema kangomba haya huna dawa mkulima asipulize korosho, unataka mkulima asizalishe korosho huna dawa anapatikana tajiri anasema bwana chukua 100,000 anakwenda kununua salfa akienda kununu salfa muda wa msimu yule aliyetoa fedha anapewa korosho unamwambia akuoneshe shamba la korosho alitoe wapi wakati yeye amemsaidia mkulima, nyie Serikali leo mnashindwa kumsaidia mkullima, kama hela yake ya korosho hajapewa unataka alime na nini? Mimi nilikuwa nataka ingewezekana ufanye uombe siku tatu tu Bungeni hapa kusiwe na posho au kitu gani tuone kama tutajaa humu. (Makofi)

SPIKA: Hiyo haikubaliki Mheshimiwa Katani.

MHE. KATANI A. KATANI: Mheshimiwa Spika, labda tungepata uchungu wa watu wa korosho ukoje siku tatu tusema hamna posho hamna nini viti hapa kama havikubaki vinane hapa, lakini kwa wakulima hawa wana dhambi gani? (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)