Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo Zilizowasilishwa katika Mkutano wa Kumi na Nne na Mkutano wa Kumi na Tano wa Bunge

Hon. Dr. Adelardus Lubango Kilangi

Sex

Male

Party

Ex-Officio

Constituent

None

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo Zilizowasilishwa katika Mkutano wa Kumi na Nne na Mkutano wa Kumi na Tano wa Bunge

MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Nami naomba kuchangia hii hoja iliyopo Mezani ambayo ni Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge kuhusu Sheria Ndogo. Nianze kwa kuwapongeza sana Kamati kwa kazi nzuri ambayo wameifanya ya kutuchambulia hizi sheria ndogo na kuona kama ziko sawasawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitajielekeza katika mapendekezo mawili niliyoyasikia kutoka kwenye michango ya Waheshimiwa Wabunge. Na la kwanza ni kwamba waandika sheria katika Wizara na taasisi mbalimbali wanaoandika hizi sheria ndogo wafanye kazi kwa karibu na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili kwa namna fulani limeanza kufanyika kwa sababu wanasheria wote wa Serikali katika Wizara na taasisi mbalimbali sasa wamefanywa kuwa ni mawakili wa Serikali na kimsingi wanafanya kazi zao chini ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Pia tumeshatengeneza mfumo wa uratibu kwa kuwaratibu hao wanasheria. Kwa hiyo, nafikiri pendekezo hili halitakuwa na changamoto kubwa ya kulitekeleza kwa sababu kimfumo na kimuundo sasa limekwisha fanyiwa kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pendekezo la pili ni lile la kuboresha viwango vya waandishi wa sheria. Kama ambavyo umeona waandishi wa sheria wanahitajika siyo tu katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali lakini hata katika Wizara na taasisi mbalimbali za Serikali kwa sababu zinajihusisha kwa namna moja au nyingine katika kuandika sheria ndogo. Suala hili la kuboresha na kupandisha viwango tumeshaliona na ninapenda nilitaarifu Bunge lako Tukufu kwamba tumeshaandaa mpango wa mafunzo na kwa kwelli sehemu fulani ya mafunzo hayo na yatakayokuwa yanahusu uandishi wa sheria yataanza katika kipindi cha miezi mitatu ijayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa hatutafanya mafunzo haya kwa wanasheria waliopo kwenye Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali peke yake, lakini kama nilivyosema, tutawahusisha wanasheria walio katika Wizara na taasisi nyingine za Serikali lakini pia tutawahusisha wanasheria wanaofanya kazi Bungeni, tutawahusisha pia wanasheria walio katika Muhimili wa Mahamaka kwa sababu hao wote kwa namna moja au nyingine wanahusika na uandishi wa sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie tu dakika moja kwa kusema Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imeshaandaa mpango na inaanza kuutekeleza ndani ya miezi mitatu ijayo ya kuanzisha chuo au taasisi ya mafunzo kwa ajili ya wanasheria wa Serikali. Tumegundua kwamba wanasheria wa Serikali pengine walikuwa wamesahaulika lakini wanahitaji taasisi yao maalum kwa ajili ya kuwafundisha haya mambo mbalimbali wanayoyahitaji ikiwemo masuala ya uandishi wa sheria. Ninatumaini mwaka kesho tutakapokutana tena hapa nadhani observations za hii Kamati zitakuwa zimebadilika. Ahsante sana.