Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya pamoja ya ziada ya Nagoya – Kuala Lumpur kuhusu Uwajibikaji Kisheria na Fidia kwa Madhara yanayoweza kutokea kutokana na matumizi ya Bioteknolojia ya Kisasa katika Kutekeleza Itifaki ya Cartagena (Nagoya – Kuala Lumpur Supplementary Protocol on Liability and Redress on Cartagena Protocol on Biosafety) pamoja na Azimio la Kuridhia Itifaki ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika kuhusu Kulinda Haki Miliki za Wagunduzi wa aina mpya za Mbegu za Mimea. (Protocal for Protection of New Varieties of Plants (Plant Breeder’s Rights) in The Southern African Development Community – SADC) pamoja na Azimio la Kuridhia Mkataba wa Marrakesh wa mwaka 2013 unaowezesha upatikanaji wa kazi zilizochapishwa kwa watu wasioona, wenye uoni hafifu au ulemavu unaomfanya mtu kushindwa kusoma (The Marrakesh Treaty to Facilitate Access to Published Work For Persons Who Are Blind, Visually Impaired or Otherwise Print Disabled)

Hon. George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya pamoja ya ziada ya Nagoya – Kuala Lumpur kuhusu Uwajibikaji Kisheria na Fidia kwa Madhara yanayoweza kutokea kutokana na matumizi ya Bioteknolojia ya Kisasa katika Kutekeleza Itifaki ya Cartagena (Nagoya – Kuala Lumpur Supplementary Protocol on Liability and Redress on Cartagena Protocol on Biosafety) pamoja na Azimio la Kuridhia Itifaki ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika kuhusu Kulinda Haki Miliki za Wagunduzi wa aina mpya za Mbegu za Mimea. (Protocal for Protection of New Varieties of Plants (Plant Breeder’s Rights) in The Southern African Development Community – SADC) pamoja na Azimio la Kuridhia Mkataba wa Marrakesh wa mwaka 2013 unaowezesha upatikanaji wa kazi zilizochapishwa kwa watu wasioona, wenye uoni hafifu au ulemavu unaomfanya mtu kushindwa kusoma (The Marrakesh Treaty to Facilitate Access to Published Work For Persons Who Are Blind, Visually Impaired or Otherwise Print Disabled)

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kujumuisha au kusema kwa kifupi kwa yale ambayo yamechangiwa. Kwanza nianze kumshukuru Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Bishara na Mazingira, Mheshimiwa Saddiq Murad na Makamu Mwenyekiti Mheshimiwa Col. Mstaafu Masoud Ally pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Viwanda, Biashara na Mazingira. Aidha, nawashukuru pia Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Eng. Joseph Mwalongo pamoja na Naibu Katibu Mkuu Balozi Joseph Sokoine na wataalam wote wa Wizara Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kushiriki na kuandaa azimio hili hadi hatua hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kimsingi wachangiaji wengi kwa pande zote mbili za Kamati ikiwepo upande wa Upinzani ni kama vile wameunga mkono Nyongeza la Azimio hili la kuhusiana na masuala ya Bioteknolojia. Kusema kweli, ingawa ilielezwa hapa kwamba tumechelewa, lakini upande wa Upinzani wamesema kwamba tulipaswa kuacha kuridhia kwa sababu tumefanya hivyo kwa haraka na pengine wadau hawakushirikishwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Azimio hili ni nyongeza tu la Azimio la Cartagena ambalo Tanzania iliridhia mwaka 2003. Nyongeza hii ilitokana na namna ambavyo hatua za uwajibikaji na ulipaji wa fidia kwa wale watakaoathirika na matumizi ya bioteknolojia ambapo kulikuwa na mvutano na kikawekwa kifungu cha 27 ili nchi ziweze kwenda kutafakari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nyongeza hii kutoka mwaka 2003 mpaka 2019 ni miaka takribani 16. Kwa hiyo, tathmini na tafakari zimefanyika sana na ndiyo maana sasa limekuja kuwekwa humu kuwa eneo au sehemu ya Azimio lile la Cartagena ambalo ilipitishwa mwaka 2000 na Tanzania tuliridhia mwaka 2003.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niwatoe mashaka kwamba ushirikiswaji haukufanyika. Siyo kweli, ushirikiswaji ulifanyika kwa kiasi kikubwa sana na kwamba hatua hii ni muhimu sana kwa sababu hatuna namna yoyote ya kuzuia madhara yanayotokana na bioteknolojia. Sisi Tanzania basically, hatujaanza kutumia bioteknolojia, lakini hatuna namna ya kuzuia kwa sababu bioteknolojia inaweza kukuathiri kwa namna nyingi; inaweza kuwa direct or indirect. Bidhaa zake tunazitumia na wapo watu inawezekana wameathirika. Kwa hiyo, kusema tusiridhie au tusite ni kuendelea kujiweka katika mazingira ambayo watu wetu wakipata madhara, hatuwezi kupata fidia au hawawezi kufidiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kwanza tumechelewa, lakini sasa tumeamua na Bunge lako limeamua kukaa na kujadili na kwa kiasi kikubwa wameunga mkono. Kwa hiyo, nawashukuru sana, akiwepo mchangiaji mmoja Mheshimiwa Eng. Chiza ambaye amezungumzia kuhusiana na suala la utafiti kwamba tafiti zimeondolewa. Kwenye ule utafiti umeweka msamaha kwa hatua za kisheria kwa utafiti katika matumizi ya bioteknolojia au shughuli za kitafiti kwa ujumla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niseme tu, pande zote; kwa upande wa Upinzani, Kamati na Waheshimiwa Wabunge wote wametoa maoni mazuri. Sisi kama Serikali tumejipanga na maoni yale yaliyotolewa tutayazingatia kwamba lazima tujenge uwezo wa wataalam kubaini madhara lakini pia jamii kupata elimu ya faida na madhara ya bioteknolojia. Maoni haya yaliyotolewa na Kamati ya Kudumu ya Bunge tumeyachukua na tutayafanyia kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya maelezo hayo, naomba kutoa hoja. (Makofi)

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naafiki.